Connect with us

News

IEBC inalenga vijana wa Gen Z katika zoezi la usajili wa wapiga kura

Published

on

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC inatarajiwa kuanza rasmi zoezi la usajili wa wapiga kura wapya kote nchini, Septemba 29 mwaka huu huku ikijiandaa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.

Mwenyekiti wa Tume hiyo, Erastus Ethekon alisema zoezi linalenga kusajili vijana zaidi ya milioni 6.3, na litazinduliwa rasmi katika kaunti ya Kajiado siku ya Jumatatu.

Ethekon alisema zoezi hilo litatekelezwa pia katika vituo vya huduma Centre, na Ofisi za Tume ya IEBC katika maeneo bunge yote 290 kote nchini ili kuhakikisha idadi kubwa ya wakenya wanasajili hasa wale ambao bado hawajasajiliwa kama wapiga kura.

“Tunalenga kusajili idadi kubwa ya wapiga kura ambazo ni vijana wa Gen Z katika zoezi ambalo litaanza rasmi siku ya Jumatatu tarehe 29 mwezi Septemba, 2025 na tunawarai wakenya wote wale ambao hawajasajiliwa kutumia nafasi hii”, alisema Ethekon.

Wakati huo huo aliweka wazi kwamba Tume ya IEBC itahakikisha uchaguzi mkuu ujao unakuwa huru na haki, wakianda na chagunzi zote ndogo nchini zitakazofanyika Novemba 27 huku akiwarai wakenya kutopuuza zoezi hilo la usajili wa wapiga kura.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending