News
IEBC yasikitishwa na idadi ndogo ya wanaojisajili
Tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC, imeeleza kusikitishwa na idadi ndogo ya wananchi wanaojitokeza kujisajili kama wapiga kura tangu kuanza kwa zoezi hilo tarehe 29 Septemba mwaka huu.
Mwenyekiti wa IEBC, Erastus Ethekon, alisema miongoni mwa changamoto zinazokwamisha usajili, ni umbali wa ofisi za tume hiyo na mchakato mrefu wa kupata vitambulisho vya kitaifa, na propaganda kwamba uchaguzi hautakuwa huru na wa haki.
Kufikia tarehe 31 mwezi Oktoba, IEBC ilisajili wapiga kura wapya 90,020 kote nchini, huku 15,619 wakihamisha kura zao, kaunti ya Mombasa ikisajili wapiga kura wapya 3,967 pekee, ikilinganishwa na lengo la wapiga kura wapya 183,000 .
Wakati huo huo Ethekon alishinikiza wakenya kupuuza madai ya wanasiasa kwamba wataiba kura zikiwemo za chaguzi ndogo.
Kwa upande wake, mkurugenzi mkuu wa tume ya IEBC, Hussein Marjan, aliwataka vijana kujitokeza kwa wingi kujisajili na kutumia haki yao ya kikatiba kuwachagua viongozi wanaowataka.
Taarifa ya mwanahabari wetu.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

