Connect with us

News

IEBC yawaidhinisha wagombea wa ubange wa Magarini

Published

on

Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC iliwaidhinishwa wagombea wa nafasi mbalimbali za changuzi ndogo zitakazoandaliwa Novemba 27 mwaka huu kabla ya kuanza rasmi kampeni

Katika kaunti ya Kilifi, wagombea zaidi ya 11 ambao wanamezea mate kiti cha ubunge wa Magarini waliwasilisha stakabadhi zao kwa Tume ya IEBC ili kuidhinishwa rasmi na kupewa cheti za kuwania wadhifa huo.

Stanley Karisa Kenga wa Chama cha DCP, Samuel Kombe Nzai wa chama cha Wiper, Furaha Ngumbao Chengo wa chama cha DNA ni kati ya viongozi walioidhinishwa na Tume ya IEBC katika ofisi cha Tume hiyo zilizoko mjini Malindi.

Wengine waliopata nafasi ya uidhinishwa siku ya Jumatano tarehe 9 mwezi Oktoba ni pamoja na Hamadi Karisa Chadi wa chama cha Roots Party, Emmanuel Kitsao Kalama wa chama cha TWAP, na John Sulubu Masha wa chama cha Kenya Social Congress.

Wagombea wengine alipangiwa zoezi hilo la kuidhinishwa siku ya Alhamis baada ya kuwasilisha stakabadhi zao na kupigwa msasa na maafisa wa IEBC ambao watasimamia uchaguzi huo mdogo wa Magarini.

Hata hivyo mgombea wa kiti hicho kupitia chama cha Federal Party of Kenya Jacob Themo Kwicha amekosa kuidhinishwa na maafisa wa IEBC baada ya cheti chake ya kugombea kiti hicho kutoka kwa chama kuonyesha kwamba anawania kiti cha uwakilishi wadi.

Cheti cha Jacob Themo Kwicha, cha chama cha Federal Party of Kenya kilichosababisha kukosa kuidhinishwa na IEBC

Tayari kampeni za uchaguzi huo mdogo wa Novemba 27, zinatarajiwa kuanza huku idara ya usalama kaunti ya Kilifi chini ya Kamishna Josphat Biwot ikiwaangaza wanasiasa hao kufanya kampeni za amani.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending