News
IEBC yawaidhinisha wagombea wa ubange wa Magarini
Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC iliwaidhinishwa wagombea wa nafasi mbalimbali za changuzi ndogo zitakazoandaliwa Novemba 27 mwaka huu kabla ya kuanza rasmi kampeni
Katika kaunti ya Kilifi, wagombea zaidi ya 11 ambao wanamezea mate kiti cha ubunge wa Magarini waliwasilisha stakabadhi zao kwa Tume ya IEBC ili kuidhinishwa rasmi na kupewa cheti za kuwania wadhifa huo.
Stanley Karisa Kenga wa Chama cha DCP, Samuel Kombe Nzai wa chama cha Wiper, Furaha Ngumbao Chengo wa chama cha DNA ni kati ya viongozi walioidhinishwa na Tume ya IEBC katika ofisi cha Tume hiyo zilizoko mjini Malindi.
Wengine waliopata nafasi ya uidhinishwa siku ya Jumatano tarehe 9 mwezi Oktoba ni pamoja na Hamadi Karisa Chadi wa chama cha Roots Party, Emmanuel Kitsao Kalama wa chama cha TWAP, na John Sulubu Masha wa chama cha Kenya Social Congress.
Wagombea wengine alipangiwa zoezi hilo la kuidhinishwa siku ya Alhamis baada ya kuwasilisha stakabadhi zao na kupigwa msasa na maafisa wa IEBC ambao watasimamia uchaguzi huo mdogo wa Magarini.
Hata hivyo mgombea wa kiti hicho kupitia chama cha Federal Party of Kenya Jacob Themo Kwicha amekosa kuidhinishwa na maafisa wa IEBC baada ya cheti chake ya kugombea kiti hicho kutoka kwa chama kuonyesha kwamba anawania kiti cha uwakilishi wadi.

Cheti cha Jacob Themo Kwicha, cha chama cha Federal Party of Kenya kilichosababisha kukosa kuidhinishwa na IEBC
Tayari kampeni za uchaguzi huo mdogo wa Novemba 27, zinatarajiwa kuanza huku idara ya usalama kaunti ya Kilifi chini ya Kamishna Josphat Biwot ikiwaangaza wanasiasa hao kufanya kampeni za amani.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

