Connect with us

International News

Iran Yafanya Mashambulizi Qatar

Published

on

Katika juhudi za kulipiza Mashambulio ya jeshi la Marekani dhidi ya vituo vya Nyuklia, Iran siku ya Jumatatu Juni 23, imevurumisha makombora na kushambulia kambi ya jeshi la Marekani ilioko Qatar, Milki za Kiarabu.

Mashambulio hayo ya hivi punde katika mzozo huo wa Mashariki ya Kati, yanazidisha wasiwasi katika eneo hilo la Ghuba.

Muda mfupi baada ya shambulio hilo, Bahrain na pia Qatar ambazo ni makao ya kambi ya kikosi cha 5th Fleet cha Jeshi la Marekani, zilisitisha mara moja safari zote za ndege katika anga zao.

Makombora hayo ya Iran yalilenga kambi ya kijeshi ya Al Udeid nchini Qatar ingawa jeshi la Marekani liliweza kuyategua makombora hayo kabla ya kusababisha maafa makubwa.

Hakuna habari zozote za majeruhi zilizotolewa kufikia sasa.

Shirika la Habari la AP liliripoti kwamba, Iran imetoa taarifa kudai kwamba makombora yaliyovurumishwa yanauzani sawa na yale yaliyotumiwa na Jeshi la Marekani kuharibu vituo vyake vya Nyuklia huko Fordow.

Hata hiyo Iran ilisema kwamba ililenga kambi hiyo la Al Ufeid ambayo iko mbali kidogo na makaazi ya watu.

Aidha makombora hayo pia yalilenga kambi ya makaazi ya jeshi la Marekani la Ain Al-Assad iliyoko eneo la magharibi mwa Iraq.

Kiongozi wa Iran Ayatollah Ali Khamenei alionya kwamba, Mashambulio hayo ya Marekani yatakuwa na athari kubwa za kiusalama sio tu kwa Marekani bali pia eneo la Mashariki ya Kati.

Isreal pia ilizidisha Mashambulio yake dhidi ya Iran kulenga gereza ambalo yaaminika limekuwa likitumiwa kuwafungia wanaharakati wa kisiasa nchini humo.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

International News

Vita dhidi ya Al-Shabab vya shika kasi Somalia

Published

on

By

Operesheni kali ya kijeshi inayoendelea nchini Somalia ambapo zaidi ya wanamgambo 33 wa kundi la Alshabab wameuawa katika eneo la Shabelle nyanda za chini za Jubaland.

Ufanisi wa operasheni hii ya hivi punde ni muendelezo wa oparesheni iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita Aprili 24 katika eneo hilo la Juba ambapo Wanamgambo 27 wa AlShabab waliuawa.

Hii ina maana kwamba Jeshi la Somali limefanikiwa kuvunja maficho muhimu ya kundi hilo, ambalo kufikia sasa ya Wanamgambo 60 wameuawa

Kwa mujibu wa vianzo vya habari hususan kutoka kwa maafisa wa usalama, operesheni hiyo inafanyika kufuatia taarifa za kijasusi kuhusu maficho ya wanamgambo hao waliokuwa wakipanga mashambulizi dhidi ya vituo muhimu na taasisi za serikali.

Wanajeshi hao walivamia ngome za magaidi hao kwa ustadi mkubwa, wakifanikiwa kudhibiti eneo hilo baada ya mapambano makali yaliyochukua muda wa saa kadhaa.

Maafisa wamesema kuwa mafanikio hayo ni sehemu ya juhudi zinazoendelea za kuimarisha usalama na kuangamiza kabisa mtandao wa Al-Shabaab ambao kwa muda mrefu umekuwa ukihatarisha amani katika maeneo mbalimbali ya Somalia na ukanda mzima wa Afrika Mashariki.

Wananchi wa eneo la Jubbaland wameelezea matumaini mapya kufuatia operesheni hiyo, wakisema kuwa hatua hiyo inaleta nuru ya kurejea kwa utulivu na maendeleo baada ya miaka ya hofu na mashambulizi ya mara kwa mara nchini.

Serikali imeapa kuendeleza msako dhidi ya wanamgambo hao hadi pale watakapokomesha kabisa vitisho vya mashambulio , huku ikiwataka wananchi kushirikiana na vyombo vya usalama kwa kutoa taarifa zitakazosaidia kudhibiti ugaidi.

Taarifa ya Billy Mongo

Continue Reading

International News

Kumbukumbu za muaji ya kimbari Rwanda

Published

on

By

Ni miaka 32 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari nchini Rwanda.

Leo, tarehe saba Aprili, raia wa Rwanda pamoja na dunia kwa ujumla wanaungana kukumbuka kuanza kwa mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, ambapo zaidi ya watu laki nane, wengi wao wakiwa jamii ya Watutsi, waliuawa ndani ya kipindi cha siku mia moja.

Tarehe hii ni ya kihistoria kwa taifa hilo ambalo miaka 32 iliyopita lilikumbwa na moja ya matukio ya kikatili zaidi katika historia ya mwanadamu.

Mauaji hayo yalichochewa na kuuawa kwa aliyekuwa rais wa Rwanda Juvenal Habyarimana, tukio lililosababisha kuzuka kwa vurugu kote nchini.

Kilichofuatia ni mashambulizi ya kimbari kati ya Wahutu na Watutsi, ambapo zaidi ya watu milioni moja wanaripotiwa kupoteza maisha katika muda wa siku mia moja.

Wanawake, wanaume na watoto walilengwa katika mashambulizi hayo yaliyopangwa, jamii zikivunjika na dunia ikishuhudia tukio hilo kwa muda bila kuchukua hatua za haraka kuzuia maafa hayo.

Katika kuadhimisha siku hii, inayojulikana kama KWIBUKA, yenye maana ya “tunakumbuka,” bendera nchini Rwanda zinapepea nusu mlingoti, huku Rais Paul Kagame akitarajiwa kuwasha mwenge wa kumbukumbu katika makavazi ya Kigali.

Hata hivyo, licha ya historia hiyo ya maumivu, Rwanda imepiga hatua kubwa katika kipindi cha miongo mitatu iliyopita, ikijijenga upya kutoka jamii iliyogawanyika hadi kuwa taifa lenye umoja, likishuhudia maendeleo ya kijamii na kiuchumi pamoja na juhudi za maridhiano na haki kwa wahanga.

Leo hii, Rwanda inasimama kama mfano kwa mataifa mengine aduniani, huku wito wa kuhakikisha mauaji ya kimbari hayajirudii tena ukiendelea kusisitizwa.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending