News
Itikadi za kidini na mafunzo ya kupotisha shuleni
Itikadi za kidini na mafunzo ya kupotisha, sasa zimeanza kupenya katika mazingira ya shule licha ya uovu huo kuonekana katika maeneo ya nyumba za ibada na kuchangia wasiwasi mkubwa kwa jamii mashinani.
Zaidi ya shule 17 katika wadi ya Sokoke eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi, zilizua gumzo baada ya shule hizo kuonekana kuwashawishi wanafunzi kukumbatia mafunzo ya dhehebu la kihindi la Krishna HOI kwa msingi kwamba linapokea msaada wa chakula kutoka kwa shirika moja lenye misingi ya Kihindi.
Miongoni mwa masharti yanayotolewa na Shirika hili ni kwamba wanaofaidika na chakula hicho ni sharti wazingatie maombi haya kabla ya kula chakula, bila ya kujali misingi yao ya kidini na utamaduni.
Na kutokana na hali ngumu na umaskini unaokithiri eneo hili la Ganze, shule nyingi zimekumbatia mpango huu na shule zinazoridhia masharti haya pia hupokea mabango haya yenye maandishi kwa lugha ya kihindi yanayopasa kukaririwa na wanafunzi.
Kulingana na masharti haya mabango haya yanapasa kutundikwa jikoni ambako maombi haya ni sharti kwa kila mwanafunzi wanapopakiliwa chakula.
Kinachoshangaza zaidi ni kwamba hata mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Kahingoni yenye zaidi ya wanafunzi 200 ambayo inakisiwa kwamba ni kati ya shule zilizokuwa zikipokea msaada huo na kukumbatia mafunzo ya dini hiyo kihindi ya Krishna HOI.

Shule ya msingi ya Kahingoni eneo la Sokoke kaunti ya Kilifi ni miongoni mwa shule zinazoendeleza Itikadi za kidini na mafunzo ya kupotisha
Japo Lengo na madhumuni ya muhisani huyu halijabainika,tayari wakaazi wengi wa eneo hili wameingiwa na hofu ya kuhusidha mpango huu na visa vya itikadi, hasa ikizingatiwa matukio ya Shakahola na Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.
Hata hivyo katika kikao na Wanahabari kuhusu hali halisi ya itikadi hizi za kidini katika mazungira ya shule, Kamishna wa kaunti ya Kilifi Josphat Biwot amesema mpango huo wa usambazaji wa chakula cha msaada kwa shule hizo usimamishwa.
Kamishna Biwot amesema walimu katika shule hizo husika watachukuliwa hatua za kisheria kwani serikali haikubaliana na itikadi za kidini shuleni.
Taarifa ya Eric Ponda
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

