News
Ofisi ya ODPP imehitimisha rasmi kesi ya Mackenzie
Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (ODPP) imehitimisha rasmi kesi yake dhidi ya mauaji ya Shakahola, ambapo Mhubiri tata Paul Mackenzie na wenzake 35 wanakabiliwa na mashtaka ya unyanyasaji, mateso na ukiukaji wa haki za watoto.
Kesi hiyo inayoendelea katika Mahakama ya watoto ya Tononika jijini Mombasa mbele ya Hakimu mkuu Nelly Chepchirchir ilianza mnamo tarehe 24 Julai 2024, na kukamilika ramsi kwa uwasilishaji wa mashahidi kutoka upande wa mashtaka.
Upande wa mashtaka ukiongozwa na Mkurugenzi msaidizi wa mashtaka ya umma, Jami Yamina, Victor Owiti, Betty Rubia, Biasha Khalifa, na Eunice Odongo katika kipindi cha kesi, waliwasilisha mashahidi 75 ambao walieleza vitendo vya unyanyasaji, mateso, na kukataliwa kwa haki ya elimu, ambayo yalifanyika katika Shakahola.
Mashahidi watatu akiwemo mtaalamu wa uchambuzi wa data kutoka kampuni ya mawasiliano ya Safaricom Dennis Muriithi walitoa ushahidi wao Mahakamani.
Muriithi amethibitisha kwamba baada ya kupata agizo kutoka kwa Mahakama walifanikiwa kufuatilia namba za simu zinazomilikiwa na Mackenzie, na kutoa taarifa za muhimu kwa uchunguzi.
Shahidi mwengine Israel Veronica, mwenye umri wa miaka 21 kutoka Chakama, mjini Malindi, ameelezea jinsi alivyolazimishwa na baba yake kuacha shule mwaka 2019, na baadaye familia yao ikahama kutoka Nairobi hadi Shakahola baada ya kuuza mali zao.
Naye Inspekta Phoebe Okomo kutoka Kitengo cha Ulinzi wa Watoto cha DCI Mombasa amesimulia kuhusu uokoaji wa watoto 27 kutoka Malindi, akielezea mazingira magumu waliyokuwa nayo watoto hao wakiwa Shakahola, ikiwemo kukosa chakula, kuteswa, na kupigwa.
Kesi hiyo itajadiliwa tena tarehe 14 Oktoba 2025 kwa ajili ya kuthibitisha kama maandiko ya kesi yameandikwa kwa ajili ya kuwasilishwa Mahakamani.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

