News
Rais Ruto azindua malipo ya bilioni 4.4 kugharamia matibabu ya wakenya kupitia SHA
Rais William Samoei Ruto amezindua malipo ya shilingi bilioni 4.4 kwa ajili ya gharama ya matibabu ya wakenya milioni 2.2 wasiojiweza chini ya mpango wa bima ya afya ya SHA.
Akizungumza katika ikulu ya Nairobi, wakati wa uzinduzi huo Rais Ruto alisema mpango huo unalenga kutoa huduma za afya bila malipo kwa wakenya wasiojiweza kifedha.
Rais Ruto alisema ni sehemu ya utekelezaji wa ajenda ya afya kwa wote na ya mageuzi mapya ya sekta ya afya nchini.
Aidha, Rais Ruto alisema hakuna Mkenya ambaye atahangaika kutokana na ukosefu wa huduma za matibabu kutokana na hali ya umasikini.

Wahudumu wa afya ya nyanjani na wakenya wahuhudhuria uzinduzi wa malipo ya shilingi bilioni 4.4 kwa ajili ya gharama ya matibabu ya wakenya milioni 2.2 wasiojiweza chini ya mpango wa bima ya afya ya SHA.
“Tuko na mahospitali elfu tisa, unaweza sasa kuenda kwa hospitali yoyote miongoni mwa hizo ili upate huduma za matibabu’’ alisema Rais Ruto.
Wakati huohuo, Rais Ruto alisema kufikia sasa ni takribani Wakenya milioni 26 ambao wamesajiliwa kwenye bima hiyo na zaidi ya milioni 5.5 tayari wanapokea huduma za matibabu kote nchini na fedha hizo zitatumika kugharamia huduma za matibabu kwenye hospitali za umma na zile zilizoorodheshwa.
‘’Hiyo pia itatusaidia kuondoa mambo ya ukora kule ndani na ufisadi’’ aliongeza Rais Ruto.
Naye waziri wa afya nchini Aden Duale alisema hospitali ambazo zitapatikana na visa vya ulaghai zitakabiliwa kisheria.
Taarifa ya Janet Shume
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

