News
Jaji wa Mahakama ya Rufaa Fred Ochieng’ Andago ameaga dunia
Idara ya Mahakama nchini pamoja na Wanasheria wanaomboleza kifo cha Jaji wa Mahakama ya Rufaa Fredrick Ochieng’ Andago aliyefariki dunia siku ya Jumatano, Septemba 17, 2025
Jaji mkuu nchini ambaye pia ni Rais wa Mahakama ya Upeo Martha Koome alimtaja Marehemu kama Jaji aliyejitolea kuitumia idara ya Mahakama kikamilifu kwa kuzingatia muongozo wa Katiba.
Naye Naibu Jaji mkuu Philomena Mwilu, amesema idara ya Mahakama imepoteza Mwanasheria aliyejitolea kutekeleza majukumu yake kwa kuhakikisha haki na sheria inalindwa.
Hata hivyo Msajali mkuu wa Idara ya Mahakama nchini Winfrida Mokaya ilisema idara ya Mahakama impoteza mtu muhimu sana kwenye masuala ya sheria, akisema Jaji Ochieng’ ataendelea kukumbwa na wengi kutokana na juhudi zake.
Jaji Ochieng’, ambaye hadi kufariki kwake, alikuwa akihudumu kama Jaji wa Mahakama ya Rufaa katika Mahakama ya Nakuru, na atakumbukwa kama afisa wa Mahakama aliyejitolea kuitumikia Mahakama kwa uadilifu na aliyechangia mageuzi mengi kwenye idara ya Mahakama
Mnamo 2003, kazi yake ilichukua mkondo wa kihistoria alipoteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu, kwani kwa miaka mingi, aliongoza vitengo na vituo muhimu, ikiwa ni pamoja na kitengo cha biashara na ushuru jijini Nairobi, pamoja na vituo vya Mahakama Kuu katika maeneo ya Kitale, Kakamega, na Kisumu.
Jaji Ochieng’ pia aliwahi kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Kisumu kabla ya kupandishwa cheo hadi katika Mahakama ya Rufaa.
Mpango ya maandalizi ya mazishi imeanza huku tarehe rasmi ya mazishi ikitarajiwa kutangazwa baadaye na familia yake
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

