Connect with us

News

Kaunti ya Kilifi yawaagiza wauguzi kusitisha mgomo na kurejea kazini

Published

on

Huku mgomo wa wauguzi wa kaunti ya Kilifi ukiingia siku yake ya pili, na kusambaratisha utaoji wa huduma za afya, Serikali ya kaunti hiyo imejitokeza na kuzungumzia suala hilo.

Kati ya lalama zilizochangia Wauguzi kushiriki mgomo ni pamoja na malimbikizi ya mishahara ya mwezi Januari na Februari mwaka wa 2021, kutopandishwa vyeo, mazingira duni ya kazi miongoni mwa masuala mengine.

Msemaji wa serikali ya kaunti ya Kilifi Jonathan Mativo alisema japo serikali ya kaunti hiyo inafahamu kuhusu malimbikizi hayo ya mishahara ikiwemo malimbikizi ya deni la zaidi ya shilingi bilioni 11, kamati maalum imebuniwa kusawazisha suala hilo.

“Tunajua kuna malimbikizi ya deni la zaidi ya shilingi bilioni 11 lakini hiyo haihusiani na masuala haya ya mgomo wa wauguzi, ndiposa tunasema kuna jopo liliundwa kuangalia suala hilo la baada ya siku 45 litatoa ripoti yake”, alisema Mativo

Mativo, aliwarai wauguzi hao kurejea kazini na kushiriki mazungumzo ya kutatua matakwa yao ili kuhakikisha huduma za afya katika hospitali na zahanati za umma, hazikumbwi na changamoto.

“Tuna waagiza wauguzi wote walio katika mgomo kurejea kazini mara moja na kushiriki mazungumzo ya kutatua matakwa yao, tunajua kwamba kuna malimbikizi ya mishahara yao ya mwezi Januari na Februari mwaka wa 2021 lakini hiyo hatuaezilipa kwa sababu kuna kesi Mahakamani na Jaji Mbaru alitoa uamuzi wa wazi kabisa kuhusu suala hilo,” alisema Mativo.

Waziri wa Afya katika serikali ya kaunti ya Kilifi Peter Mwarogo alitoa onyo kali kwa Muungano wa wauguzi hao kwamba utachukuliwa hatua za kinidhimu iwapo utawashurutisha wauguzi watakaorejea kazini ama kukatiza huduma kwenye hospitali za kaunti.

“Taratibu za kupandisha wauguzi vyuo ziko na tunawaambia wauguzi warudi kazini na wale ambao wanaendelea na kazi hatutarusu watishie ama mtu kutatiza shughuli za hospitali, wale watapatikana tutawachukulia hatua na hata kuwafungulia mashtaka Mahakamani”, alifafanua Mwarogo.

Akizungumzia mgomo huo wa wauguzi, Mwenyekiti wa bodi ya huduma za umma kaunti ya Kilifi Albert Muturi alisema licha ya kufanya vikao kadhaa na Muungano wa wauguzi, na hata wauguzi 530 kupandishwa vyeo, hawafai kugoma.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending