National News
Mahakama Kuu ya Malindi Yahairisha Kesi ya Ulaghai
Mahakama kuu mjini Malindi kaunti ya Kilifi imeahirisha kwa mara ya mwisho uamuzi wa kesi ya madai ya ulaghai wa fedha unaodaiwa kutekelezwa na Kenneth Njoroge Maina kwa mtalii Garallin Chiara.
Hakimu mkaazi wa Mahakama hiyo, Nkurrunah Namunyak amesema uamuzi wa kesi hiyo ulikuwa tayari ila mshtakiwa ameshindwa kufika Mahakamani kwa mara sita mfululizo kwa madai ya changamoto za kiafya.
Kulingana na stakabadhi za kesi hiyo, Maina anadaiwa kumlaghai Chiara shilingi 124,800 za kusimamia huduma za usafiri wa mtalii huyo kutoka Malindi hadi mbuga ya wanyama ya Tsavo na kukosa kutimiza ahadi yake.
Kupitia Wakili wa Maina, hapo awali alieleza Mahakama kwamba alikuwa amepata asilimia 70 ya fedha za mlalamishi na akataka kumrudishia Chiara fedha zake japo Mahakama hiyo ilidai kwamba wakili wa mshtakiwa alishindwa kuieleza Mahakama kuhusu ugonjwa wa mshtakiwa.
Uamuzi wa kesi hiyo unatarajiwa kutolewa mnamo siku ya Jumatatu tarehe 17 mwezi Machi mwaka huu.
National News
Umoja wa mataifa wapunguza bajeti yake kwa bola milioni 577
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amependekeza kupunguzwa kwa bajeti ya umoja huo ya mwaka ujao kwa dola milioni 577, hatua ambayo itapunguza asilimia 18 ya kazi.
Akizungumza mbele ya kamati ya bajeti ya Baraza kuu la umoja wa mataifa, Guterres alisema umoja huo bado haujapokea mchango wa karibu dola milioni 900 kutoka kwa wanachama mwaka huu wa 2025.
Umoja wa mataifa unapendekeza bajeti ya dola bilioni 3 kwa mwaka 2026, ikiwa na upungufu wa asilimia 15 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka huu.
Umoja wa Mataifa unakabiliwa na mgogoro wa kifedha uliosababishwa pakubwa na hatua ya Marekani kutolipa ada yake, kutokana na sera mpya za Rais Donald Trump.
Hatua hii ya umoja wa mataifa huenda ukachangia changamoto kubwa kwa mataifa wanachama hasa yanayotegemea pakubwa juhudi za umoja huo katika masuala mbalimbali ikiwemo usalama.
Editor's Picks
Bangi Yanaswa Daraja la Sabaki – Malindi, Kaunti ya Kilifi
Maafisa wa Usalama wamenasa shehena ya Bangi katika daraja la Sabaki, Mjini Malindi Kaunti ya Kilifi, iliyokuwa imefichwa kwenye makasha ndani ya basi lililokuwa likisafiri kitoka Lamu kwenda Mombasa.
Basi hilo lilisimamishwa na Maafisa wa usalama katika kizuizi Cha Polisi kilichoko daraja hilo kwa shughuli ya kawaida ya ukaguzi wa magari na mizigo, ambapo magunia mawili ya bangi hiyo yalipatikana yamefichwa katika sehemu ya Mizigo ndani ya basi hilo.
Dereva na Kondakta wa basi hilo, mali ya kampuni ya mabasi ya Tawakal, walikamatwa, ingawa abiria anayeaminika ndiye mwenye kusafirisha bangi hiyo alitotoka mtego huo na bado anatafutwa na Maafisa Polisi.
Waliokamatwa sasa wanazuiliwa katika kituo cha Polisi cha Mjini Malindi huku uchunguzi zaidi unapoendelea.
Maafisa hao wanasema, walipata vidokezo kuhusiana na bangi hiyo ambayo bado haijajulikana thamani yake.
Katika siku za hivi karibuni, Daraja hilo la Sabaki limekuwa chini ya oparesheni kali ya maafisa wa usalama kutokana kuongezeka Kwa idadi ya vyombo vya usafiri, hasa Malori ambayo yaaminika kutumika kwa zaidi kwa biashara haramu kutoka Kaunti za Tana River na Lamu kuingia Kaunti za Kilifi na Mombasa.
Dereva huyo na Kondakta wake watafikishwa mahakamani hivi karibuni huku maafisa wa Polisi wakitia wito kwa wanachi kutoa habari zitakazosaidia kumtia nguvuni mshukiwa mkuu.

