News
Mchungaji akamatwa kwa kuwalazimisha watoto kufunga kula katika kijiji cha Dera,Kilifi
Idara ya usalama katika kaunti ya Kilifi imeanzisha uchunguzi baada ya kumkamata Mhubiri tata Kamanza Mwatela Kwa tuhma za mahubiri potovu ya kidini katika kijiji cha Dera eneo bunge la Kilifi Kaskazini.
Katika opareseheni hiyo, polisi walifanikiwa kuwaokoa watoto watano walikuwa wamedhohifika baada ya kulazimishwa kufunga kula na kunywa.
Afisa mkuu wa idara ya DCI kaunti ya Kilifi Robert Kiinge alisema Mhubiri huyo wa kanisa la Jesus Ministry alikuwa akiendesha ibada katika nyumba aliyokodi katika kijiji hicho baada ya kuhama kutoka mjini Malindi.
“Tunaendelea na uchunguzi kubaini kiini hasa cha Mchungaji huyo maana huwezi lazimisha watoto kufunga kula na kunywa”, alisema Kiinge.
Kwan upande wake Afisa wa watoto eneo la Kilifi Kazkazini Warren Apopo alisema baada ya kuwahoji watoto hao walibaini kwamba watoto walikuwa wakienda shule kama kawaida na hawakuwa wakifunga kula.
Apopo alifafanua kwamba huenda kuna tatizo la kifamilia katika hilo boma kwani Mchungaji huyo alikuwa amekaribishwa na mama mmoja aliyemuombea hadi akapona.
“Tuliwahoji watoto na kukagundua kwamba walikuwa wanaenda shule na pia hawakuwa wanafunga lakini kuna tatizo hapo kwa boma tunashuku tu mchungaji alikuwa na mahusiano na mama mmoja ndio kuna hizi tuhma”, alisema Apopo.
Wakaazi eneo hilo walisema walikuwa wakitilia shaka mafunzo ya mchungaji huyo kwa kuwazuilia watoto na kuwashawishi wazazi na watoto kupuuza masomo.
Kulingana na mzee wa kijiji hicho Alphonce Kahindi, mchungaji huyo aliwasili katika kijiji cha Dera mwezi wa pili mwaka wa 2025, na kuanzisha ibada zake katika nyumba aliyokodi kabla ya kuanza kuwashawishi watoto hao kufunga kula na kunywa.
Kahindi alidokeza kuwa hali hiyo ilimlazimu kuripoti kwa idara ya usalama ambao walifika na kuwaokoa watoto hao huku wawili kati yao wakiwa wamedhoofika zaidi kiafya baada ya kufunga kwa siku 6.
“Kuna mchungaji ambaye amefungia watoto ndani ya nyumba kwa ajili ya kuomba, sasa watoto wako humo na jana ilikuwa ni siku ya sita, hawajakula hawajakunywa, ikabidi nimpigie simu chifu wa Sokoni na nikapigia madam D.O, ikabidi madam D.O atume tayari gari yake na askari, tukakuja jana jioni na tukampata huyo mchungaji”, alisema Kahindi.
Tukio hilo linajiri wakati ambapo washukiwa kadhaa wanaendelea kuzuiliwa na polisi kuhusiana na madai ya mauaji ya watu katika eneo la Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi kufuatia ushawishi wa dini potofu.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

