Sports
Michael Olunga Aondoka Al-Duhail
Sasa ni rasmi kwamba mshambulizi wa timu ya soka Harambee Stars Engineer Michael Ogada Olunga ametangaza kuachana na waajiri wake kilabu ya Al- Duhail ya Qatar
Mwamba huyo alijiunga na kilabu hiyo msimu wa mwaka 2021 akitokea Keyshiwa Reysol ya japana na mpaka sasa amefanikiwa kuibuka mfungaji bora kwenye kilabu hiyo akifunga magoli 130.
Kupitia kwenye tuvuti ya kilabu hiyo Al-Duhail imeweza kumshukuru nyota huyo ambaye amefunga magoli 12 msimu huu na kuchangia mengine mawili katika mechi 19 ambazo amechezea kilabu hiyo
Nyota huyo amewahi shinda kiatu cha dhahabu akiwa mfungaji bora mwaka 2021-22 na magoli 22.
Vilabu vingine ambazo amechezea ni pamoja na Girona ya Uhispania,Djugardens ya Sweeden,Zhicheng ya Uchina na Keyshiwa Reysol ya Japan.
Mpaka sasa haijawekwa wazi kilabu yake mpya.
Sports
Klabu ya Arsenal guu moja kuingia hatua ya Nusu fainali Klabu bingwa baada ya ushindi dhidi ya Sporting
Sports
Wakili George Kithi akabidhiwa rasmi Cheti cha uenyekiti wa bodi ya Michezo marufu kama Sports Arts and Social Development Fund (SASDF)
Waziri wa Wizara ya Masuala ya Vijana, Uchumi bunifu na Michezo, Salim Mvurya, ameshudia hafla rasmi ya kukabidhiwa uenyekiti wa Bodi ya Sports, Arts and Social Development Fund (SASDF) kutoka kwa Luteni Jenerali Mstaafu Jackson Tuwei kwenda kwa Mheshimiwa wakili George Kithi. Hafla hiyo ilifanyika, jijini Nairobi hii leo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Waziri Mvurya alimpongeza Luteni Jenerali (Mstaafu) Tuwei kwa uongozi wake wa mfano na kujitolea kwake katika kipindi chake cha utumishi. Alibainisha kuwa chini ya uongozi wake, bodi hio iliimarika na kuwa taasisi imara na yenye mwitikio zaidi katika kusaidia na kuendeleza vipaji vya Wakenya.
Aidha, Waziri alieleza imani yake kwa uongozi wa Mheshimiwa wakili George Kithi, akimhakikishia ushirikiano na msaada kamili kutoka kwa Wizara katika kutekeleza majukumu ya Bodi kwa kipindi chake cha miaka mitatu.
SASDF inaendelea kuwa nguzo muhimu katika kulea na kukuza vipaji vya Kenya, pamoja na kuimarisha hadhi ya nchi kimataifa kupitia michezo na uchumi wa ubunifu. Kupitia uwezeshaji wa wanamichezo, wasanii na wadau wa utamaduni, mfuko huo unachangia pakubwa katika ukuaji wa sekta za michezo na ubunifu nchini.

