Connect with us

News

Murkomen akemea maandamano ya kupinga kupanda kwa bei ya mafuta

Published

on

Serikali imekosoa maandamano yaliyoandaliwa siku ya Jumatatu Mei 18,2026 kote nchini ya kupinga kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Serikali imesema haitakubali baadhi ya watu kuendelea kuharibu na kupora mali ya umma, ikisema watakaopatikana watakabiliwa kikamilifu kwani maafisa wa kupambana na ghasia wako kila sehemu kuhakikisha usalama unaimarishwa pamoja na kulinda mali ya umma na biashara za wakenya.

Katika kikao na Wanahabari kilichojumuisha wakuu wa usalama nchini akiwemo Inspekta Jenerali wa polisi, Naibu Inspketa Jenerali wa polisi Eliud Lang’at, Katika katika Wizara ya usalama wa ndani Raymond Omollo miongoni mwa wengine, Waziri wa usalama wa ndani Kipchumba Murkomen alisema wakati wa maandamano hayo watu wanne walithibitishwa kupokeza maisha yao.

Waziri Murkomen alisema watu wengine 30 walijeruhiwa kufuatia makabiliana na maafisa wa polisi huku watu 348 wakitiwa nguvuni na  kutokana na kushiriki maandamano ambayo hayajaidhinishwa na maafisa wa polisi.

“Ni jambo la kusikitisha kwamba watu wanne walipoteza maisha yao kufuatia maandamano hayo, lakini ningependa kuwaambia wananchi maandamano ya kupinga kupanda kwa bei ya mafuta haitasaidia, ni wadau wa sekta ya uchukuzi wa umma kufanya mazungumzo na viongozi wa serikali na mwafaka utapatikana”, alisema Murkomen.

Murkomen pia aliwalaumu viongozi wa kisiasa nchini, akisema ndio wanaochangia taifa kushuhudia vurugu na maandamano ya kila mara hali ambayo taifa limekuwa likipoteza raslimali nyingi.

Aidha alieleza kwamba maandamano sio njia mwafaka ya kutatua tatizo la ongezeko la bei ya mafuta nchini huku akisisitiza kwamba serikali inalishuhulikia suala hilo kupitia ushirikiano wa Hazina ya kitaifa, pamoja na Wizara ya Kawi na Wizara ya uchukuzi na kwmaba wanaendelea na mikakati ya kuhakikisha suala hilo linatatuliwa kupitia mazungumzo na wadau wa sekta ya uchukuzi nchini.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending