Connect with us

News

Wanaharakati wanataka barabara ya Mombasa-Malindi kukamilishwa kujengwa

Published

on

Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu katika eneo la Pwani wamefanya maandamano ya amani wakilalamikia hali mbovu ya barabara ya Mombasa-Malindi.

Wanaharakati hao wanasema ukarabati wa barabara hiyo hasa eneo la Mtwapa umechukua muda mrefu kukamilika na kuchangia kudorora kwa uchumi wa eneo la Pwani huku magari yanayotumia barabara hiyo yakiendelea kuharibika kila mara.

Wakiongozwa na Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Vocal Africa Hussein Khalid, Wanaharakati hao walikosoa mwendo wa polepole wa ujenzi wa barabara hiyo, wakisema umegeuka kuwa tishio kwa usalama na shughuli za kiuchumi.

“Kila kukicha magari yanaharibika barabara ni mbovu, kwa hivyo tunaiambia serikali tunataka hii barabara iishe haraka iwezekanavyo”, alisema Khalid.

Wanaharakari wafunga barabara ya Mombasa -Malindi wakilalamikia ubovu wa barabara hiyo

Kwa upande wake, Khelef Khalifa wa shirika la MUHURI amekosoa jinsi miradi ya maendeleo katika eneo la Pwani inavyotekelezwa kwa mwendo wa kujikokota, akisema hali hiyo imelemaza utoaji wa huduma muhimu kwa wananchi.

“Tukienda Feri, watu ambao wanavuka kwa feri ni laki nne kwa siku na magari elfu 20, hakuna daraja kila kitu kinatoka hapa kinafanywa huko kila kitu kinafanywa huko polisi wenyewe wanalalamika ni utovu wa usalama sasa tumeanza kupeleka barua wanaanza kujazajaza kwa mawe”, alisema Khelef

Wanaharakati hao sasa wanaitaka serikali kuharakisha ukamilishaji wa barabara hiyo ili kupunguza ajali, msongamano wa magari pamoja na kuboresha shughuli za biashara kati ya kaunti za Pwani

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wadau wa sekta ya uchukuzi wasitisha mgomo wao

Published

on

By

Maafisa wa sekta ya uchukuzi wameahirisha mgomo wao baada ya mazungumzo yaliyoongozwa na Rais William Ruto katika ikulu ya Mombasa.

Maafisa hao wakiongozwa na rais wa Muungano wa wamiliki wa matatu Albert Karagacha wamesema kuwa mengi ya masuala waliokuwa nayo ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta nchini yameangaziwa kwa kina na rais Ruto.

Karagacha amewataka wahudumu wa sekta ya uchukuzi wa umma pamoja na wamiliki wa magari ya uchukuzi wa mizigo kuhakikisha wanarudisha magari yao barabarani, akisema masuala waliowasilisha kwa rais yameangaziwa

Akizungumza mda mfupi baada ya kufanya kikao na rais William Ruto mjini Mombasa, Karagacha amesema serikali imekuwa kiangazia kwa kina masuala mbali mbali yanayohusu sekta ya uchukuzi nchini.

Aidha amesema iwapo bado serikali itakuwa inajikokota katika kufanikisha masuala waliojadiliana basi wataitisha mazungumzo zaidi na Wizara husika ili kuafikiwa kwa ajenda zao huku akisema japo suala la mzozo wa mafuta sio jambo la Kenya pekee lakini taifa inawajibu wa kusaidia wananchi wake.

Wakati huo huo Karagacha amewataka wakenya kutoingiza siasa katika suala la kupanda kwa bei ya mafuta nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Mshukiwa wa ulanguzi na usafirishaji wa watoto anyimwa dhamana

Published

on

By

Mahakama ya Shanzu imemnyima dhamana mshukiwa wa ulanguzi wa watoto zaidi ya 20.

Mahakama imeagiza mshukiwa huyo kuzuiliwa rumande ili kuwawezesha maafisa wa polisi kukamilisha uchunguzi wao.

Mahakama imeelezwa kwamba mshukiwa huyo Almasi Rama Amos mwenye umri wa miaka 27 alikamatwa na maafisa wa upelelezi kutoka kitengo cha kupambana na ulanguzi wa binadamu na ulinzi wa watoto (AHTCPU) pamoja na maafisa wa idara ya upelelezi wa Jinai kutoka kaunti ya Mombasa.

Kukamatwa kwake kufuatia wiki kadhaa za uchunguzi kuhusu ripoti za unyanyasaji wa watoto zinazowalenga wasichana wadogo walio katika mazingira magumu.

Rama, anayetuhumiwa kwa kujihusisha na kundi linalodaiwa kuwa la ulanguzi wa watoto na dhulma za kingono na kufikishwa katika Mahakama ya Shanzu kufuatia operesheni ya kiusalama iliyoidhinishwa na maafisa hao.

Rama alipatikana katika mtaa wa Nguu Tatu eneo la Concordia katika kaunti ndogo ya Kisauni akiwa na watoto watatu wa kike.

Mahakama imeelezwa kuwa mshukiwa anadaiwa kuendesha “vituo vya uokoaji” katika kaunti za Mombasa na Kilifi kwa kujifanya kuwalea na kuwapa ushauri.

Kulingana na uchunguzi vituo hivyo vilikuwa vikitumika kama msingi wa dhulma za kingono na unyanyasaji wa watoto.

Alipokamatwa, mshukiwa aliwaongoza maafisa hadi kituo chengeni eneo la Ribe katika eneo bunge la Rabai, ambapo maafisa wa upelelezi waliwaokoa watoto 19 wa jinsia ya kike na kufikisha jumla ya waathiriwa waliookolewa kufikia ishirini na wawili (22).

Mbele ya Mahakama ya Shanzu tarehe 21 Mei, 2026, mshukiwa amekabiliwa na mfululizo wa mashtaka, ikiwemo unajisi, biashara ya watoto kwa madhumuni ya kuwadhulumu kingono pamoja na unyanyasaji wa watoto ambapo amekana mashtaka hayo.

 Kesi hiyo imepangwa kutajwa Juni 8, 2026.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

Trending