News
Wanaharakati wanataka barabara ya Mombasa-Malindi kukamilishwa kujengwa
Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu katika eneo la Pwani wamefanya maandamano ya amani wakilalamikia hali mbovu ya barabara ya Mombasa-Malindi.
Wanaharakati hao wanasema ukarabati wa barabara hiyo hasa eneo la Mtwapa umechukua muda mrefu kukamilika na kuchangia kudorora kwa uchumi wa eneo la Pwani huku magari yanayotumia barabara hiyo yakiendelea kuharibika kila mara.
Wakiongozwa na Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Vocal Africa Hussein Khalid, Wanaharakati hao walikosoa mwendo wa polepole wa ujenzi wa barabara hiyo, wakisema umegeuka kuwa tishio kwa usalama na shughuli za kiuchumi.
“Kila kukicha magari yanaharibika barabara ni mbovu, kwa hivyo tunaiambia serikali tunataka hii barabara iishe haraka iwezekanavyo”, alisema Khalid.

Wanaharakari wafunga barabara ya Mombasa -Malindi wakilalamikia ubovu wa barabara hiyo
Kwa upande wake, Khelef Khalifa wa shirika la MUHURI amekosoa jinsi miradi ya maendeleo katika eneo la Pwani inavyotekelezwa kwa mwendo wa kujikokota, akisema hali hiyo imelemaza utoaji wa huduma muhimu kwa wananchi.
“Tukienda Feri, watu ambao wanavuka kwa feri ni laki nne kwa siku na magari elfu 20, hakuna daraja kila kitu kinatoka hapa kinafanywa huko kila kitu kinafanywa huko polisi wenyewe wanalalamika ni utovu wa usalama sasa tumeanza kupeleka barua wanaanza kujazajaza kwa mawe”, alisema Khelef
Wanaharakati hao sasa wanaitaka serikali kuharakisha ukamilishaji wa barabara hiyo ili kupunguza ajali, msongamano wa magari pamoja na kuboresha shughuli za biashara kati ya kaunti za Pwani
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

