News
Mwili wa mtoto Keziah wasafirishwa Tarasaa kaunti ya Tanariver kwa mazishi
Jamaa na Marafiki walifika eneo la Mwezang’ombe kaunti ya Kilifi kuuaga mwili wa Kezia Matuki mwenye umri wa miaka saba na aliyekuwa mwanafunzi wa gredi ya pili ambaye mwili wake ulipatikana wiki chache zilizopita ukiwa umetupwa nje ya boma lao eneo hilo la Kwa Nzai, kabla ya kuusafirisha kwa ajili ya mazishi ambayo yameratibiwa kufanyika Jumamosi 16, Mei 2026 katika eneo la Tarasaa kaunti ya Tana River.
Waliotoa rambirambi zao kwa familia walilaani kitendo hicho, wakimtaja Keziah kama mtoto ambaye alikuwa akishirikiana na watoto wenzake vyema akiwa shuleni na hata nyumbani.
Vilevile, walisema kifo kimezima ndoto ya Kezia ambaye alikuwa mwanafunzi mwenye bidii shuleni.
“Kezia atakumbukwa na wengi kutokana na ucheshi wake na namna alivyokuwa akiiishi na watoto wenzake na hatujawahi kuskia ripoti zozote mbaya kumhusu kama za kuwachokoza wenzake” walisema waombolezaji

Mwili wa Keziah Matuki unaombolezwa na wengi kufuatia kifo chake tatanishi
Kwa upande wake naibu gavana wa kaunti ya Kilifi Flora Chibule alilaani kitendo cha kuuawawa kwa Kezia na kutaka uchunguzi kuharakishwa ili haki ipatikame kwa familia na aliyehusika akabiliwe kisheria.
“Hili ni kisa cha kusikitisha Sana na asasi husika zinapaswa kuharakisha uchunguzi na aliyehusika awajibishwe kisheria ili iwe funzo kwa wengine” Alisema Chibule
Awali ripoti ya upasuaji wa mwili wa Keziah ulibaini kuwa aliuawa kwa kunyongwa.
Ripoti hiyo pia ilibaini kuwa alivunjwa shingo na kisha kunajisiwa.
Daktari mkuu wa hospitali ya rufaa ya Kilifi, Gilbert Angore, alisema sampuli zaidi zilipelekwa katika maabara ya serikali kwa uchunguzi wa kina.
Haya yanajiri huku mshukiwa wa mauaji hayo Dennis Otieno Oduor akiendelea kuzuiliwa rumande huko Shimo la Tewa kaunti ya Mombasa, uchunguzi unapoendelezwa.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Aisha Jumwa akihama rasmi chama cha UDA
Mgombea wa kiti cha ugavana wa kaunti ya Kilifi Aisha Jumwa amekihama rasmi chama cha UDA, akisema atatangaza baadaye mwelekeo atakaochukua wa kisiasa.
Jumwa alitoa tangazo hilo katika kikao na Wanahabari kilichofanyika katika makaazi yake, eneo la Kakuyuni huko Malindi kaunti ya Kilifi leo siku ya Alhamis.
Hatua ya Jumwa ilijiri baada ya kuwepo na tetesi kwamba alikuwa na mipango ya kuhama chama hicho kutokana na sintofahamu za kisiasa ndani ya chama cha UDA kuhusu msimamo wake wa kisiasa wa kuwania nafasi ya ugavana wa Kilifi.
Jumwa alilalamika kwamba alikuwa akinyanyaswa na baadhi ya viongozi hata kutimuliwa katika Ikulu ya rais licha ya kupambana katika kampeni za rais Ruto mwaka wa 2022, akionekana kumlaumu rais Ruto kwa kutomjali tena hata baada ya kusimama na yeye kisiasa.
Kiongozi huyo alikashfu vikali kutengwa katika mikutano ya UDA licha ya kuwa mwandani wa rais Ruto na pamoja na kufanyikisha miradi ya serikali mashinani, akisema tangu atangaze mchakato wa kuwania kiti cha ugavana wa Kilifi mwaka wa 2027, amekuwa akipitia masaibu mengi.
Hii sio mara ya kwanza kwa Jumwa kukihama Chama cha UDA na kurejea kwenye chama hicho, lakini hatua aliyoichukua sasa itabadili masimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi.
Itakumbukwa kwamba Jumwa amekuwa mwandani wa karibu wa rais William Ruto, lakini hatua aliyoichukua huenda ikabadili msimamo wa kisiasa kaunti ya Kilifi na Pwani kwa jumla.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Mahakama ya Kilifi yaagiza kuzuiliwa Washukiwa 7 wa mauaji
Mahakama ya Kilifi imeagiza kuzuiliwa kwa siku 14 washukiwa 7 wanaotuhmiwa kuhusika katika kifo cha mwanamke mmoja aliyekuwa na umri wa miaka 65, ambaye aliuwawa kwa tuhma za uchawi katika eneo la Malomani eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi.
Washukiwa hao Gilbert Karisa Changawa, Selvestar Changawa Kahindi, Elizabeth Jackson Ngala, Dhahabu Kithi Kombe, Dzendere Palu Kalama, Agness Changawa na Kadzo Ngombo Bienge watazuiliwa katika kituo cha Bamba wakati uchunguzi ukiendelea.
Kulingana na Afisa mpelelezi kutoka kitengo cha DCI ameeleza mahakama kwamba ilikuwa mnamo tarehe 27 mwezi huu ambapo walipokea tarifa kwamba dama changawa alikuwa amekatwa kichwa na kuuwawa na watu wasiojulikana usiku huo.
Afisa mpelelezi pia ameeleza kuwa washukiwa ambao ni wanafamilia,siku kabla ya tukio husika walikuwa wameandaa kikao cha kudumisha Amani baada ya kifo kilichokuwa kimetokea kwa kijana mmoja mtoto wa mmoja kati ya washukiwa aliyefariki kaunti ya Mombasa baada ya kupigwa kwa tuhma za wizi.
Kutokana na kifo cha kijana huyo wanafamilia hao walimtuhmu dama kwamba ndiye aliyekuwa amemroga kijana huyo na kusababisha kifo hicho cha gafla, ambapo usiku huo Dama aliuwawa nyumbani kwake.
Washukiwa watarudishwa mahakamani tarehe 13 mwezi Agosti mwaka huu baada ya uchunguzi kukamilika.
Taarifa ya Teclar Yeri

