News
Usalama umeimarishwa kabla ya ziara ya Rais Ruto, Kilifi
Serikali imesema usalama umeimarishwa katika kaunti ya Kilifi kabla ya ziara ya rais William Ruto juma lijalo katika halfa ya uzinduzi wa ujenzi wa uwanja wa kitaifa katika eneo la Tezo na miradi mingine zaidi ya 20 kaunti ya Kilifi.
Kamishna wa kaunti ya Kilifi David Wanyonyi na Katibu katika Idara ya ulinzi nchini Dkt Patrick Mariru, wamesema maafisa wa usalama wanashika doria katika kila sehemu ya kaunti ya Kilifi.
Akizungumza na Wanahabari baada ya ukaguzi wa matayarisho ya ujenzi wa uwanja wa Ronald Ngala katika eneo la Tezo kaunti ya Kilifi, Katibu katika Wizara ya ulinzi nchini Dkt Patrick Mariru amesema mipango na mikakati imeandaliwa.
Kamishna wa kaunti ya Kilifi David Wanyonyi amesema vitengo mbalimbali vya kiusalama vinashirikiana kuhakikisha visa vya utovu wa usalama vinakomeshwa ili kufanikisha shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Katika katika Wizara ya ulinzi Dkt Patrick Mariru afanya ukaguzi wa ujenzi wa uwanja wa Ronald Ngala, eneo la Tezo kaunti ya Kilifi
Wanyonyi alisisitiza kwamba vikundi vya kihalifu vitakabiliwa kwani maafisa hao wanashika doria pia katika miji mkuu ikiwemo Kilifi, Malindi, Watamu na Mtwapa huku onya kukomeshwa visa vya dhulma za kijinsia.
Kwa upande wake Kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa ambaye pia ni Mbunge wa Kilifi Kaskazini Owen Baya amesema ziara ya rais Ruto ni mafanikio makubwa kwa wakaazi wa Kilifi kwani zaidi ya miradi 20 itazinduliwa.
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

