Connect with us

News

Naibu rais akosoa upinzani kuhusu bei ya mafuta nchini

Published

on

Naibu rais Profesa Kithure Kindiki amerejea tena kaunti ya Kilifi ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kuendeleza ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo katika kanda ya Pwani.

Hata hivyo ziara hiyo imeonekana kuangazia zaidi suala tata la kupanda kwa bei ya mafuta nchini ambalo linadaiwa kusababishwa na vita vinavyoendelea katika mashariki ya Kati.

Akitetea hatua ya serikali, naibu rais alisema tayari serikali imechukua hatua madhubuti na za haraka kupunguza ushuru wa mafuta, ili kumkinga mwananchi kutokana na athari za mfumuko wa bei za bidhaa na kuongezeka kwa gharama ya maisha.

Akihutubiwa wananchi katika eneo bunge la Rabai, Professa Kindiki alionekana kuulenga upinzani kwa kuingiza siasa katika suala la mafuta, akikosoa mpango wao wa kuandaa maandamano akisema sio suluhu kwa tatizo hilo.

Hatua ya hii ya Kindiki ilionekana kupokea msukumo kutoka kwa viongozi wakuu ndani chama cha UDA wakiongozwa na katibu wa Chama Omar Hassan Sarai ambaye alikosoa mpango ya upinzani kuandaa maandamano.

Jumatano ya aprili 15, 2026, Rais William Ruto alitangazi mipango ya serikali kutatua tatizo la kupanda kwa bei ya mafuta nchini kwa kupunguza ushuru wa mafuta.

Viongozi wengine walioandamana na naibu rais katika eneo bunge la Rabai akiwemo mwenyekiti wa bodi ya barabara nchini Aisha Jumwa, mbunge wa eneo hilo Kenga Mupe vile vile mwenyekiti wa bodi ya hazina ya michezo, sanaa na maendeleo Wakili George Kithi, waliitaka serikali kuangazia masuala mbali mbali yanayowakumba wakaazi wa kilifi, ikiwemo uhaba wa maji safi, ukosefu wa dawa hospitalini na uvamizi wa ndovu kwa wakaazi wa eneo bunge la Ganze.

Awali naibu rais alitembelea miradi mbali mbali eneo hilo ikiwemo uzinduzi wa mradi wa nyumba za bei nafuu, na nyumba za malazi kwa wanafunzi wa taasisi ya ufundi, na ukaguzi wa mradi wa kituo cha huduma eneo la Shikaadabu huko Rabai.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending