Connect with us

News

Naibu rais akosoa upinzani kuhusu bei ya mafuta nchini

Published

on

Naibu rais Profesa Kithure Kindiki amerejea tena kaunti ya Kilifi ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kuendeleza ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo katika kanda ya Pwani.

Hata hivyo ziara hiyo imeonekana kuangazia zaidi suala tata la kupanda kwa bei ya mafuta nchini ambalo linadaiwa kusababishwa na vita vinavyoendelea katika mashariki ya Kati.

Akitetea hatua ya serikali, naibu rais alisema tayari serikali imechukua hatua madhubuti na za haraka kupunguza ushuru wa mafuta, ili kumkinga mwananchi kutokana na athari za mfumuko wa bei za bidhaa na kuongezeka kwa gharama ya maisha.

Akihutubiwa wananchi katika eneo bunge la Rabai, Professa Kindiki alionekana kuulenga upinzani kwa kuingiza siasa katika suala la mafuta, akikosoa mpango wao wa kuandaa maandamano akisema sio suluhu kwa tatizo hilo.

Hatua ya hii ya Kindiki ilionekana kupokea msukumo kutoka kwa viongozi wakuu ndani chama cha UDA wakiongozwa na katibu wa Chama Omar Hassan Sarai ambaye alikosoa mpango ya upinzani kuandaa maandamano.

Jumatano ya aprili 15, 2026, Rais William Ruto alitangazi mipango ya serikali kutatua tatizo la kupanda kwa bei ya mafuta nchini kwa kupunguza ushuru wa mafuta.

Viongozi wengine walioandamana na naibu rais katika eneo bunge la Rabai akiwemo mwenyekiti wa bodi ya barabara nchini Aisha Jumwa, mbunge wa eneo hilo Kenga Mupe vile vile mwenyekiti wa bodi ya hazina ya michezo, sanaa na maendeleo Wakili George Kithi, waliitaka serikali kuangazia masuala mbali mbali yanayowakumba wakaazi wa kilifi, ikiwemo uhaba wa maji safi, ukosefu wa dawa hospitalini na uvamizi wa ndovu kwa wakaazi wa eneo bunge la Ganze.

Awali naibu rais alitembelea miradi mbali mbali eneo hilo ikiwemo uzinduzi wa mradi wa nyumba za bei nafuu, na nyumba za malazi kwa wanafunzi wa taasisi ya ufundi, na ukaguzi wa mradi wa kituo cha huduma eneo la Shikaadabu huko Rabai.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Tume ya IEBC imepongeza zoezi la usajili wa wapiga kura wapya

Published

on

By

Naibu Mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC Fahima Araphat amesema zoezi la usajili wa wapiga kura wapya linaendelea vyema licha ya changamoto mbalimbali.

Akizungumza katika ukumbi wa Kibaoni mjini Kilifi kaunti ya Kilifi kwenye hafla ya ushirikishaji wadau katika kutoa maoni kuhusu namna zoezi hilo linavyotekelezwa kaunti ya Kilifi, Araphat alisema kufikia Aprili 15 walikuwa wamesajili watu milioni 1.3.

Araphat pia alisema wakenya wanaendelea kujitokeza katika zoezi hilo na mikakati ifaayo imewekwa kuhakikisha wananchi wote wanasajiliwa kuwa wapiga kura ili washiriki uchaguzi mkuu ujao wa 2027 na kujitenga na madai kuwa IEBC inaegemei mrengo flani wa kisiasa.

‘’Sisi kama tume tutahakikisha kuna uwazi katika usajili huu na hata wakati wa kuandaliwa kwa uchaguzi mkuu na tunaomba Wakenya wajitokeze kwa wingi kusajiliwa kuwa wapiga kura kabla ya kukamilika Aprili 28’’ Alisema Araphat

Wakati huohuo, Araphat akigusia suala la uratibu wa mipaka, alisema tume ya IEBC haiwezi kufanya uratibu huo kwa sasa ila mikakati inawekwa kuhakikisha unatekelezwa.

Naye meneja wa uchaguzi wa kaunti ya Kilifi Juma Musa Juma alitoa wito kwa wadau mbalimbali kushirikiana na IEBC ili fanikisha zoezi hilo la usajili wa wapiga kura wapya akitaja eneo bunge la Magarini kama ambalo linaongoza kwa usajili huo.

‘’ Tunahitaji ushirikiano wa kila mtu na idara ili zoezi ili litekelezwe kama lilivyoratibiwa’’ Alisema Musa

Kwa upande wake mwakilishi wa wadi ya Kibarani Moses Furaha Kea, alitoa wito kwa IEBC kuhakikisha idara inayohusika na usajili wa vitambulisho inaharakisha katika utoaji ili wananchi waweze kujisajili kuwa wapiga kura.

Nao wananchi waliohudhuria hafla hiyo waliitaka IEBC kufika mashinani ili kusajili idadi kubwa ya wapiga kura na kuwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kusajiliwa huku kamanda wa polisi eneo bunge la Kilifi Kaskazini Stanley Tunui na naibu kamishna wa Kilifi Kaskazini Samuel Mutisya wakisema idara ya usalama iko imara katika kuhakikisha usalama unaimarishwa vilivyo.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mshukiwa wa dawa za kulevya akamatwa Mombasa

Published

on

By

Maafisa wa kitengo cha kupambana na dawa za kulevya eneo la Pwani wamemkamata mshukiwa mmoja raia wa kigeni anayehusishwa na mtandao wa usafirishaji wa dawa za kulevya.

Mshukiwa huyo Okwara Chimezie Emmanuel, raia wa Nigeria, anaaminika kuwa sehemu ya mtandao mpana wa usambazaji wa dawa za kulevya aina ya Heroin katika ukanda wa Pwani.

Kukamatwa kwake kulifuatia taarifa za kijasusi, ambapo maafisa wa usalama kwa ushirikiano na maafisa wa DCI walifanya operesheni maalum katika eneo la Mafisini, Kadzandani kaunti ya Mombasa.

Wakati wa msako huo, maafisa hao walifanikiwa kunasa kiasi kikubwa cha Heroin kilichokuwa kimefichwa kwenye mafungu tofauti, ikiwa na thamani ya takriban shilingi milioni 30.

Polisi wanasema uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo cha dawa hizo pamoja na kuwakamatwa kwa washirika wengine wanaodaiwa kuhusika na biashara hiyo haramu, wakiwemo raia wa Kenya wanaoshukiwa kusaidia katika usafirishaji wa dawa hizo.

Mshukiwa anatarajiwa kufikishwa Mahakamani huku maafisa wa Idara ya upelelezi wa jinai DCI wakitarajiwa kuomba muda zaidi wa kukamilisha uchunguzi wao.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending