News
NPSC hatimaye yatangaza kuajiri maafisa 10,000 wa polisi
Tume ya kitaifa ya huduma ya polisi (NPSC) hatimaye imetangaza usajili wa maafisa 10,000 wa polisi, na kumaliza mzozo wa muda mrefu kati yake na huduma ya kitaifa ya polisi (NPS).
Katika notisi iliyochapishwa katika gazeti moja la kila siku nchini, NPSC ilialika waenye nia ya kutuma maombi kupakua fomu za uajiri mtandaoni, kuzijaza, na kujiwasilisha katika vituo vilivyoteuliwa ili kuzingatiwa.
Zoezi hilo la nchi nzima limepangwa kuanza Oktoba 3 hadi Oktoba 9, 2025, katika vituo 416 vya usajli.
Zoezi hilo litalenga raia wa Kenya walio na umri wa kati ya miaka 18 na 28, walio pata alama ya chini ya D+ katika cheti cha mtihani wa kitaifa wa shule za sekondari (KCSE).
Kulingana na taarifa iliyotiwa saini na afisa mkuu mtendaji wa NPSC Peter Leley, wanaotuma maombi lazima wawasilishe vyeti halisi vya masomo na vitambulisho vyao vya kitaifa katika vituo vya kuajiri.
Tangazo hilo linafuatia wiki za mvutano kati ya NPSC na NPS kuhusu mchakato wa kuajiri.
Tume hiyo hapo awali ilishinikiza kuwepo kwa mtindo mpya unaohitaji waliotuma maombi kuorodheshwa kabla ya kuhudhuria zoezi la uhakiki.
Hata hivyo, pendekezo hilo lilitupiliwa mbali, na kuruhusu wote waliotuma maombi hayo kujiwasilisha siku ya usajili wakiwa na fomu zilizojazwa ipasavyo.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni
Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali
Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.
Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.
Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.
Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.
Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.
Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke
Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.
Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.
Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.
Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.
Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.
Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.
Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

