News
Polisi wawarai wananchi kuwa makini dhidi ya wachungaji potovu wa kidini
Idara ya usalama kaunti ya Kilifi imewarai wakaazi kuwa waangalifu dhidi ya Wachungaji potovu waliojitokeza na kuwapotosha wananchi kwa misingi ya kidini.
Afisa mkuu wa idara ya upelelezi wa jinai DCI katika kaunti ya Kilifi Robert Kiinge, alisema itikadi potovu za kidini itakomeshwe iwapo wananchi watakuwa mstari wa mbele kuwaripoti watu wanaowashuku kuwa na itikadi hizo.
Katika kikao na Wanahabari ofisini mwake mjini Kilifi, Kiinge aliwarai wazazi na jamii kwa jumla kufuatilia mienendo ya watoto ili kuzuia kupotoshwa katika itikadi za kidini, akisema kuna haja ya jamii kuwa makini.
“Kuna chipuza watu ambao wanapatiana mafunzo ya kidini ambazo haziandamani na mahubiri ambayo sisi tunajua, naomba mkiona mtu ambaye anaendeleza maneno ambayo hayaandamana na mafunzo ya vitabu tafadhali walete kwenye ofisi za usalama”, alisema Kiinge.
Wakati huo huo amedokeza kwamba vitengo mbalimbali vya kiusalama viko mashinani kuendeleza oparesheni za kijasusi ikiwemo kwa viongozi wa kidini kuhusu vyeti vyao wa masomo ya thiolojia na stakabadhi waliozo nazo ili kudhibiti mafundo potovu.
Kauli yake imejiri baada ya Mchungaji Kamanza Mwatela wa kanisa la Jesus Ministry kuzuiliwa na maafisa wa polisi kwa tuhma za kuendeleza itikadi potovu za kidini sawa na washukiwa kadhaa wanaohusishwa na mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

