Connect with us

News

Bi Rachel azindua mpango wa “lishe bora” shuleni

Published

on

Ofisi ya mke wa Rais Bi Rachel Ruto, imezindua mpango wa lishe bora kupitia utoaji wa maziwa kwa watoto wa shule kama sehemu ya mpango wa kuboresha afya na kuongeza nguvu kwa watoto ili waweze kuendelea na masomo yao shuleni bila changamoto zozote.

Akingumza katika Shule ya msingi ya Kachororoni eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi, Bi Rachel alisema mpango huo wa Feed One End Hunger ambao umefanikishwa kwa ushirikiano na Bodi ya Maziwa nchini KDB na Muungano wa ushirika wa maziwa, Meru utadhibiti utapiamlo kwa watoto.

Bi Rachel Ruto alisema wanafunzi wengi nchini ambao wanatoka kwenye familia zisizojiweza hasa kifedha wamekuwa wakisitisha masomo yao kutokana na njaa na utapiamlo kutokana na ukosefu wa lishe bora.

“Afya ya mtoto ni muhimu sana na ikiwa mpango huu wa lishe bora utakumbatiwa, wanafunzi wengi shuleni watafanya vyema katika masomo yao”, alisema Bi Rachel Ruto.

Kwa upande wake Katibu mkuu katika Wizara ya Kilimo nchini Jonathan Mueke ambaye alikuwa ameandamana na Bi Rachel Ruto aliupongeza mpango huo akiutaja kama hatua muhimu ya kufanikisha elimu shuleni.

Naye Naibu Gavana wa kaunti ya Kilifi Flora Mbetsa Chibule alisema tangu kuzinduliwa kwa mpango wa lishe shuleni kaunti ya Kilifi, wanafunzi wengi wamekuwa wakijiunga na shule mbalimbali ikilinganishwa na miaka ya nyuma na kuahidi kushirikiana na ofisi ya mke wa rais Bi Rachel Ruto katika kuhakikisha unafikishwa vilivyo.

Hata hivyo Mbunge wa Ganze Kenneth Kazungu Tungule alitoa wito kwa Rais William Samoei Ruto kujenga barabara ya Kilifi – Ganze – Bamba ili kuimarisha shughuli za uchukuzi eneo hilo.

Kauli ambayo iliungwa mkono na Mwakilishi wa Kike kaunti ya Kilifi Getrude Mbeyu, ambaye alisema eneo bunge la Ganze lina raslimali nyingi na huenda Ganze ikawa eneo tajiri zaidi nchini iwapo raslimali hizo zitatumika ipasavyo na kuipongeza Serikali kuu kupitia Wizara ya Utalii na wanyamapori nchini kutoa kima cha shilingi milioni 60 za fidia kwa wakaazi wa kaunti ya Kilifi walioathiriwa na wanyamapori.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending