Connect with us

News

Odinga awaalika wakenya kwenye kumbukumbu za Sabasaba

Published

on

Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga amewaalika wakenya kujumuika naye kati kumbukumbu za maandamano ya siku ya Sabasaba katika uwanja wa Kamukunji jijini Nairobi.

Odinga alisema hatua hiyo ni kuwakumbuka wale waliopigania mfumo wa vyama vingi nchini ambao kulingana naye mfumo huo ulifaulu japo bado kuna mambo mengi ambayo yanahitaji kulainishwa.

Itakumbukwa kuwa Odinga alikuwa miongoni mwa waliopanga siku ya maandamano ya Sabasaba ya kwanza nchini, mnamo Julai 7, 1990.

Odinga alisema yuko tayari kuadhimisha miaka 35 ya siku hii.

Kinara huyo wa ODM alisema uwanja wa Kamukunji jijini Nairobi umebeba historia ya kipekee kutokana na matukio ya wakati huo, ambapo waliowasili katika Sabasaba ya kwanza walikabiliwa na maafisa wa usalama, baadhi walipoteza maisha na mamia wakijeruhiwa katika vita vya kupigania siasa za vyama vingi.

Wakati huo huo kundi la wahuni lilivamia kikao kilichokuwa kikihutubiwa na makundi ya kinamama katika ofisi za tume ya kutetea haki za kibinadam KHRC Jijini Nairobi jumapili 6, Julai 2025.

Kinamama hao walikuwa wamewasili katika ofisi za tume hiyo ili kuzungumzia siku ya Sabasaba na walilazimika kusitisha kikao hicho huku mali na bidhaa nyingine muhimu zikiibwa.

Baadhi ya wanawake waliovamiwa katika makao makuu ya tume ya KHRC Nairobi

Wanahabari waliokuwa sehemu hiyo pia walivamiwa na kukimbilia usalama wao huku kinamama hao wakilazimika kuandaa kikao hicho sehemu tofauti baadaye.

Hata hivyo tume hiyo ya KHRC ililaani tukio hilo na kumtaka inspekta jenerali wa polisi nchini Douglas Kanja kufanya uchunguzi na kuwakamata waliohusika na uvamizi huo

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending