News
Ripoti ya upasuaji wa maiti yabainisha kilichomuua polisi,Haiti
Upasuaji wa maiti ya Kennedy Mutuku Nzuve afisa wa polisi aliyefariki nchini Haiti umebaini kuwa alifariki kutokana na majeraha yanayoambatana na ajali ya barabarani.
Upasuaji wa mwili ulifanyika siku moja baada ya mwili wa afisa huyo kurejeshwa nchini Kenya kutoka nchini Haiti.
Mwili wa afisa huyo ulipokewa na familia yake katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa JKIA jijini Nairobi mwendo wa saa tatu jioni siku ya Ijumaa Septemba 26, 2025.
Nzuve alifariki Agosti tarehe 31 kwenye doria ya usalama nchini Haiti, na sasa familia yake inasema hatua ya mwili wa Nzuve kurejeshwa nchini imeleta afueni.
Nzuve ni miongoni mwa maafisa watatu wa polisi wa Kenya waliofariki wakiwa kwenye oparesheni nchini Haiti, katika mpango wa kimataifa wa usaidizi wa usalama unaoungwa mkono na umoja wa kimataifa.
Awali kuliibuka mkanganyiko kuhusu hatma ya afisa mwengine wa polisi Benedict Kabiru ambaye alikuwa miongoni mwa mafisa waliopelekwa nchini Haiti.
Mkuu wa sheria aliiambia mahakama kuwa hana ufahamu kuwa afisa huyo wa polisi alifariki dunia nchini Haiti, kinyume na matamshi ya rais William Ruto katika kikao cha baraza la umoja wa mataifa jijini New York nchini Marekani.
Kabiru, aliyetumwa nchini Haiti chini ya ujumbe wa msaada wa usalama wa kimataifa (MMS) alishukiwa kuuawa na magenge yenye silaha mnamo mwezi machi 2025.

Maafisa wa polisi wa Kenya wakishika doria nchini Haiti.(picha kwa hisani)
Miezi kadhaa baadaye, huduma ya kitaifa ya polisi nchini ilikuwa bado haijathibitisha kifo chake, ikisema juhudi za kumtafuta zingali zinaendelea.
Familia ilifika mahakamani ikitaka maelezo, ikidai maelezo hayo alizuiliwa na maafisa kutoka ofisi ya mwanasheria mkuu.
Mawakili wanaowakilisha familia hiyo, Jumatano 25, Septemba 2025, waliambia mahakama kwamba kukiri hadharani kwa Rais William Ruto kuwa Kabiru alikuwa miongoni mwa maafisa waliofariki Haiti, kunachukuliwa kuwa ushahidi.
“Ikiwa taarifa ya rais ni sahihi, basi inatupilia mbali ombi la habari kwa kuwa uthibitisho tayari umefanywa katika ngazi ya juu,” mahakama ilisikiza.
Wakati rais Ruto alitoa taarifa kwa umma katika mkutano wa Umoja wa Mataifa, Mwanasheria mkuu alisisitiza kuwa haijapokea taarifa kama hizo kutoka kwa utawala wa polisi.
Mkanganyiko huu, walalamishi walipinga na kusema ni madai ambayo yanahitaji ufafanuzi wa haraka.
Hata hivyo mkuu wa sheria aliomba muda zaidi ili kupata taarifa zaidi.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

