News
Umoja wa upinzani waahidi kuungana licha ya pingamizi
Umoja wa upinzani umetangaza kwamba utaunga mkono mmoja wao ambaye atapambana na Rais William Ruto wakati wa uchaguzi mkuu ujao wa mwaka wa 2027.
Viongozi wa Umoja wa upinzani ambao walihudhuria mkutano wa kitaifa wa wajumbe wa chama cha Peoples Liberation Party PLP, ulioongozwa na Kinara wake Martha Karua, viongozi hao wa upinzani wameapa kusalia pamoja.
Akizungumza baada ya Chama hicho cha PLP kumpa tiketi ya kupeperusha bendera ya chama hicho kwenye kinyang’anyiro cha wadhfa wa urais wakati wa uchaguzi mkuu ujao, Karua alisema atambandua uongozi rais Ruto kuwa rais wa muhula mmoja.
Viongozi hao hata hivyo waliweka wazi msimamo wao wa kusalia pamoja na kumteua mmoja wao atakayepeperusha bendera ya umoja wa upinzani ili kumbandua rais Ruto mamlakani wakati wa uchaguzi mkuu mwaka wa 2027.

Viongozi wa umoja wa upinzani pamoja na wafuasi wa chama cha PLP wakati wa uzinduzi wa chama
Viongozi hao wa umoja wa upinzani ni pamoja na Kalonzo Musyoka wa chama cha Wiper, Martha Karua wa PLP, Rigathi Gachagua wa DCP, Eugine wa Wamalwa wa DAP-Kenya, na Justine Muturi wa Democratic Party.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

