News
Serikali yahimizwa kuwachunguza viongozi wa kidini wa itikadi potovu
Kutokana na kuongezeka kwa mafundisho ya itikadi potovu katika madhehebu mbalimbali nchini, sasa serikali imehimizwa kuanza kuwatathmini upya na kuwachunguza wachungaji wote nchini.
Aliyekuwa Mwakilishi wadi ya Gongoni kaunti ya Kilifi Albert Kiraga alitoa tahadhari kwa serikali, akisema ni lazima ilifikirie upya suala hilo kwani linatishia maisha ya jamii nyingi kutokana na matukio ya kutisha katika kijiji cha Kwa Binzaro kaunti ya Kilifi.
Kiraga alizitaka asasi za kiusalama pamoja na mamlaka zengine nchini kuanzisha mchakato mpya wa kuwachunguza wachungaji wote nchini iwapo stakabidhi zao za kidini zinaambatana na mafundisho wanayotoa kwa waumini wao.
Akizungumza na Wanahabari, Kiraga alisema tukio la hivi majuzi katika msitu wa Shakahola na kijiji cha Kwa Binzaro na sasa katika eneo la Kaloleni ambapo mtu mmoja aliyejiita Kasisi alionenkana akicheza densi juu ya mti huku waumini wakigaagaa kwenye matope wakiimba na kupiga makofi.
Kwa upande wake Mhubiri Dkt Dorcas Chebet Juma, ambaye pia ni Mhadhiri wa chuo kikuu cha Pwani alisisitiza umuhimu wa elimu ya dini miongoni mwa wachungaji na ujuzi wa kidini kwa waumini, akisema hatua hiyo itakomesha itikadi za kidini na mafunzo potovu.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

