Connect with us

News

Serikali yasema vitambilisho elfu 400 havijachukuliwa kwa ofisi za umma

Published

on

Serikali imetangaza kwamba zaidi ya Vitambulisho vya kitaifa elfu 400 kote nchini havijachukuliwa na wenyewe licha ya kutuma maombi ya kutafuta stakabadhi hiyo muhimu ya kitaifa.

Katibu katika Idara ya uhamiaji nchini Belio Kipsang, alisema licha ya maafisa wa umma kuhakikisha wanawataka wakenya ambao hawajachukua Vitambulisho vyao vya kitaifa bado kuna changamoto za kuwafikia watu hao.

Akizungumza na Wanahabari baada ya kushiriki zoezi la upinzi wa miti katika siku ya Mazingira nchini, Kipsang aliwahimiza wakenya ambao bado hawajachukua Vitambulisho vyao vya kitaifa kutembelea ofisi husika na kuchukua stakabadhi hiyo.

Katibu huyo wa idara ya uhamiaji nchini, alisema changamoto hiyo imesababisha zoezi endelevu la usajili wa wapiga kura inaloendelezwa na Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC kushuhudia idadi ndogo ya wakenya wanaojitokeza kusajiliwa.

Wakati huo huo alidokeza kwamba serikali itashirikiana na maafisa tawala ikiwemo machifu kuhakikisha vitambulisho hivyo vya kitaifa vinawafikia wenyewe bila changamoto.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni

Published

on

By

Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali

Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.

Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.

Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.

Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.

Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.

Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke

Published

on

By

Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.

Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.

Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.

Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.

Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.

Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.

Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Trending