News
Serikali yatangaza mpango wa kuongeza mgao wa mafuta kwa magari ya polisi
Serikali imetangaza mpango wa kuongeza mgao wa mafuta ya Petroli na diseli ya kila mwezi kwa magari ya polisi kutoka lita 450 za sasa hadi lita 650, ili kupunguza changamoto za kiutendaji zinazowakabili maafisa wa usalama kote nchini.
Waziri wa Usalama wa Ndani, Kipchumba Murkomen, alitoa ahadi hiyo wakati wa mkutano wa Jukwaa la Usalama uliofanyika katika Kaunti ya Homa Bay, baada ya maafisa kulalamikia uhaba wa mara kwa mara wa mafuta unaosababisha magari ya polisi kusimama kabla ya mwezi kuisha.
Kwa mujibu wa Murkomen, marekebisho hayo yatafanywa chini ya mpango unaoendelea wa ukodishaji wa magari ya polisi.
Murkomen alikiri changamoto hizo zipo na kubainisha kuwa uhaba wa mafuta umesababisha wananchi kuwa na dhana potovu kuhusu mienendo ya polisi.
“Maafisa wetu wa polisi wanapowaambia wananchi kwamba ‘gari haina mafuta, hatuwezi kuja,’ watu hufikiria afisa anaomba hongo, lakini si kweli,” alisema Murkomen.
Waziri huyo alifafanua kuwa hali ni mbaya zaidi katika maeneo ya mashinani ambapo maafisa hulazimika kusafiri umbali mrefu ili kwenda kuchukua mafuta.
“Kwa mfano, askari wa polisi wa Kibish anaposafiri hadi Kitale kuchukua mafuta, akirudi mgao huo haudumu hata siku kumi. Baada ya hapo gari hubaki limeegeshwa hadi mwezi uishe,” aliongeza Murkomen.
Ili kutatua tatizo hilo, Murkomen alisema serikali haitaimarisha mgao huo pekee hadi lita 650, bali pia itasambaza vituo vya mafuta kwa ukaribu zaidi.
Alitaja Marsabit na Moyale kama miongoni mwa maeneo ambayo hivi karibuni yatakuwa yakipata mafuta kwa karibu badala ya kusafiri hadi miji ya mbali kama Nanyuki.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

