Connect with us

News

Tungule:Baadhi ya wenye timbo Jaribuni hawajaruhusiwa kuchimba madini

Published

on

Mbunge wa Ganze katika kaunti ya Kilifi Kenneth Kazungu Tungule amesema baadhi ya wawekezaji katika eneo la Jaribuni kaunti ya Kilifi wanaendelea kufungiwa timbo zahadi watakapokamilisha ahadi ya ujenzi wa barabara sehemu hiyo.

Akizungumza katika kipindi cha Coco Asubuhi Tungule alisema kwa sasa barabara inayoelekea kwenye timbo hizo imewekwa lami umbali wa kilomota 8 pekee, ikiwa imesalia kilomita moja.

Tungule aliesema ushirikiano baina ya wananchi na viongozi umefanikisha juhudi za kushinikiza wawekezaji sehemu hiyo kutekeleza ujenzi wa barabara sehemu hiyo.

“Lakini sasa waziri alipokuja viwanjani na akaona vile hali ilivyokuwa pia akakubaliana na sisi akasema nisawasawa hao wawekezaji ni lazima waweze kutengeneza hiyo barabara ndio maana tumefika pale tumefika, na bado kuna wengine ambao hawajafungua timbo zao tunatarajia pia hao wakitaka kurudia biashara zao wanafaa kuchukua kilimota moja yao”, alisema Tungule.

Awali wakaazi wa eneo la Jaribuni waliandamana na kufunga barabara inayoelekea katika timbo hizo wakilalamikia vumbi linalochangiwa na barabara mbovu.

Vile vile walidai afya ya wakaazi imezorota kutokana na vumbi linalochangiwa na malori ya kubeba madini sehemu hizo.

Ujenzi wa barabara ya Jaribuni kuelekea kwenye timbo za madini.

Hali hii ilichangia serikali kuu kupitia waziri wa madini na uchumi wa bahari Ali Hassan Joho pamoja na gavana wa kaunti ya Kilifi kuagiza timbo hizo kufungwa mara moja hadi wawekezaji watakapoweka lami barabara hizo.

Kuhusu matatizo yanayokumba wakaazi katika eneo bunge lake ikiwemo suala la uhaba wa maji, Tungule alisema ujio wa rais Kilifi umempa taswira kamili ya changamoto hizo akiamini kuwa rais William Ruto ataziangazia.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending