News
Stanley Kenga kupeperusha bendera ya DCP-Magarini
Mwanasiasa Stanley Kenga Karisa imejiunga rasmi na Chama cha DCP kinachoongozwa na Rigathi Gachagua.
Kenga amejiunga na Chama hicho ili kugombea ubunge wa Magarini kaunti ya Kilifi utakaoandaliwa Novemba 27 mwaka huu baada ya kushurutishwa kujiondoa katika kinyang’anyiro hicho kupitia chama cha UDA.,
Akizungumza baada kukabidhiwa tiketi ya DCP na Kinara wa chama hicho Rigathi Gachagua, Kenga alipongeza uamuzi wa Chama cha DCP kwa kumpa nafasi ya kugombea ubunge wa Magarini, akisema wakaazi wa Magarini wako na nafasi nyengine katika uchaguzi huo mdogo.
“Wakati milango ilipofungwa ile ng’ambo ya pili hapa DCP, mlitufungulia milango, mkatupokea na tunashukuru. Kwa sababu mmepekea nafasi kwa jamii ya Magarini tuwezekuwa kwa debe kwa huu uchaguzi mdogo ambao unakuja tarehe 27 mwezi wa Novemba, ninasema kwamba tuko tayari na tutachukua kiti cha Magarini kupitia DCP”, alisema Kenga.
Wakati huo huo aliahidi kuhakikisha Chama cha DCP kinashinda uchaguzi huo mdogo wa Magarini, huku akiwarai wafausi wake kutorudi nyuma katika kupigania demokrasia.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

