News
Wahadhiri waanza mgomo wa kitaifa
Muungano wa Wahadhiri wa vyuo vikuu nchini (UASU) wameanza mgomo wao licha ya Hazina ya kiaifa kutoa shilongi bilioni 2.5 kwa ajili ya kutekeleza awamu ya pili ya mkataba wa makibaliano wa CBA wa 2021-2025.
Wahadhiri hao walisitisha kazi zao Jumatano Septemba 17, 2025 wakidai kuwa madai yao ya kifedha bado hayajatimizwa kama walivyokubaliana serikali.
Katibu wa UASU tawi la Nairobi, Dkt. Maloba Wekesa, alisema serikali imeshindwa kutimiza ahadi yake, akisisitiza kwamba wahadhiri wataendelea na mgomo.
Alibainisha kwamba shilingi bilioni 7.9 za malimbikizo chini ya CBA ya mwaka 2017 bado hazijalipwa licha ya Mahakama kuu mwenzio Machi mwaka 2025 kuagiza suala hilo kutekelezwa kikamilifu.
Wekesa alidai kwamba wafanyakazi wamesalia kama ombaomba wakati ambapo awamu ya pili ya malipo yao ilipaswa kulipwa licha yao kuipa serikali muda wa siku 7 kutekeleza ahadi yao baada ya kuichelewesha kwa muda wa miezi 3.
“Katika 2017-2021 tulikuwa na CBA sawa. Iliichukua serikali miezi 36 kuandika makubaliano. Tulinyimwa nyongeza ya kila mwaka. Mahakama zikaamuru utekelezaji. Tarehe 25 Machi 2025, mahakama ikaamua kwa upande wetu”, alisema Wekesa.
Aliongeza kuwa serikali ilikuwa imeahidi kutekeleza kikamilifu CBA ila kumekuwa na kimya tangu hapo huku akiongeza kuwa masuala ya afya ya wahadhiri wa UoN hayakuchukuliwa kwa uzito ilhali uongozi ulipaswa kushughulikia masuala hayo muhimu.
Kwa upande wake Katibu wa tawi la Nairobi wa Chama cha Wafanyakazi wa vyuo vikuu (KUSU), Peter Waita, aliongeza kuwa wahadhiri wamenyimwa haki yao ya msingi.
Taarifa ya Elizabeth Mwende
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

