Connect with us

News

Wakaazi wahimizwa kushirikiana na asasi za kiusalama

Published

on

Naibu Chifu wa Shella mjini Malindi kaunti ya Kilifi Nicodemus Mwayele ametoa wito kwa wenyeji kushirikiana na asasi za usalama ili kuyakabili magenge ya kihalifu ambayo yanazidi kutekeleza visa vya uhalifu maeneo mbalimbali ya mji huo.

Akizungumzia katika kikao cha umma cha kutoa maoni kuhusu namna ya kuyakabili magenge hayo, ambacho kiliandaliwa eneo la Muyeye ,Pentagon na kuwaleta pamoja Maafisa tawala, Wanaharakati na Wananchi, Mwayele alisema magenge hayo yanazidi kuchipuka hali ambayo inaendelea kuwatia hofu Wananchi.

Mwayele alisema watoto wengi eneo hilo hawaendi Shule kutokana na utumizi wa dawa za kulevya.

Kwa upande wa baadhi ya Wananchi walilalamikia hali ya Wazazi kuzembea katika malezi ya watoto wao huku wengine wakiinyoshea Idara ya usalama kidole cha lawama wakidai imetepetea katika kukabiliana na wahalifu mjini Malindi.

Wakaazi wa Shella mjini Malindi kaunti ya Kilifi wahudhuria vikao vya kukusanya maoni ya umma kuhusu usalama

Nao baadhi ya wanaharakati wakiongozwa na Victor Kaudo na Famau Mohamed Famau walidai kwamba Kituo cha kupeana dawa aina ya Methadone katika hospitali ya Kaunti ndogo ya Malindi kinachangia Kwa ongezeko la Vijana wanaotumia dawa za kulevya.

Vilevile, waliitaka oparesheni ya kuwarudisha watoto shuleni kurejeshwa kwani Idadi kubwa ya watoto hawaendi shuleni.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending