News
Zoezi la kutoa chanjo kung’oa nanga Julai 5
Wizara ya Afya imetangaza kampeni ya kutoa Chanjo bila malipo kote nchini katika juhudi za kukabiliana na maradhi ya ukambi, Homa ya tumbo na Surua.
Zoezi hilo la siku 10 linatarajiwa kuanza Julai 5 mwaka huu hadi Julai 14.
Afisa wa masuala ya Chanjo kaunti ya Kilifi Christine Mataza, na mwenzake wa Afya ya Umma Amos Ndenge wamesema zaidi ya watoto elfu 200 walio chini ya umri wa miaka mitano watapokea chanjo ya ukambi na Surua.
Aidha wamesema kwamba zaidi ya Chanjo elfu 200 za Homa ya Matumbo itapeyanwa kwa zaidi ya watoto elfu 600 wa kati ya miezi tisa hadi miaka 14 katika kaunti ya Kilifi.
Chanjo hizo ambazo hutolewa kila baada ya miaka mitano, mwaka huu itaendeshwa katika sehemu za masoko, na shule, kinyume na miaka ya nyuma ambapo zoezi hilo lilikuwa likitekelezwa nyumba hadi nyumba.
Homa ya tumbo husababishwa na matumizi ya maji machafu na Mazingira machafu huku Kenya ikiwa ni Taifa la tano barani Africa kuanzisha Chanjo mpya ya kukabiliana na Huma ya tumbo, ukambi na Surua barani Afrika
Taarifa ya Eric Ponda
News
Polisi wanachunguza tukio la wizi dhidi ya raia wa kigeni
Maafisa wa Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza tukio la wizi dhidi ya mtalii wa kigeni lililotokea katika eneo la Nyali
Kulingana na ripoti ya maafisa wa polisi, mtalii huyo mwenye umri wa miaka 51 ambaye ni raia wa Marekani, anadai kulaghaiwa na kisha kushambuliwa na kundi la wanaume aliyokutana nao muda mfupi kabla ya tukio.
Ripoti hiyo imeeleza kwamba mnamo mwezi Aprili 9 mwaka huu, raia huyo wa kigeni akiwa katika mkahawa mmoja eneo la Nyali jijini Mombasa, alikutana na mwanaume aliyejitambulisha kama Alex, ambaye alimshawishi kuelekea katika nyumba ya Airbnb iliyoko karibu na mkahawa huo.
Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kwamba alipofika katika chumba hicho, alikumbana na wanaume wengine watano waliokuwa wakimsubiri ambapo mlango ulifungwa na kisha akashambuliwa na kulazimishwa kutoa pesa na vitu vya thamani.
Wahalifu hao walitoroka na mali mbalimbali ikiwemo simu ya rununu, kompyuta mpakato (laptop), fedha taslimu pamoja na fedha za kigeni na pia walifanikiwa kutoa pesa kutoka kwenye kadi zake za benki kwa njia ya udanganyifu.
Maafisa wa polisi kutoka Bamburi kwa kushirikiana na maafisa wa upelelezi wa DCI Nyali walifika eneo la tukio na kuanza uchunguzi, ingawa hadi sasa hakuna mtu aliyekamatwa wala mali iliyopatikana.
Kesi hiyo imewekwa chini ya uchunguzi zaidi huku juhudi zikiendelea kuwabaini na kuwakamata wahusika wa tukio hilo.
Taarifa ya Mwanahabari wetu
News
Polisi eneo la Likoni-Mombasa inachunguza kifo cha mwanamke
Idara ya usalama eneo la Likoni kaunti ya Mombasa imesema inachunguza kifo cha mwanamke mmoja aliyefariki katika mtaa wa senti kumi.
Mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Mutungi alisema mwanamke huyo anadaiwa kupoteza maisha wakati wakiwa nyumbani kwa mwanamme anayesemekana kuwa mchumba wake.
Taarifa za awali ziliarifu kuwa marehemu alikuwa mgonjwa na anadaiwa alifika hospitalini kusaka matibabu japo hakupata huduma na kurejea nyumbani bila kutibiwa.
Inasemekana baadaye mchumba wake alioondoka kwenda kazini na kumwacha chini ya uangalizi wa mwanamke mwengine katika ploti hiyo.
Hali yake inadaiwa kuzorota na hatimaye kuaga dunia.
Maafisa wa usalama walisema wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha kifo hicho.
Mwili wa marehemu unahifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya Coast general kwa uchunguzi zaidi.
Taarifa ya Mwanahabari wetu

