Connect with us

News

Askofu Mwero: Mizozo ya ardhi inafaa kukomeshwa Pwani

Published

on

Viongozi wa kidini katika ukanda wa Pwani wamejitokeza na kushinikiza kuchukuliwa kwa hatua za haraka kuhusu jinsi ya kukomesha changamoto zinazoathiri maisha ya wananchi mashinani.

Mwenyekiti wa Muungano wa Makanisa nchini NCCK tawi la Pwani Askofu Peter Mwero alisema migogoro ya ardhi, mihemko ya kisiasa, ukiukaji wa katiba, ukabila miongoni mwa masuala mengine yanafaa kukomeshwa.

Akizungumza katika kikao cha kutathmini masuala mbalimbali ya kaunti ya Kwale, Askofu Mwero alisema ongezeko la visa vya dhuluma za kijinsia katika jamii vinafaa pia kukomeshwa ili kuiwezesha jamii kuishi kwa amani.

“Haya ni mambo ambayo sio mazuri katika jamii yetu katika mambo ya maendeleo, itabidi viongozi wa dini zote kuingalia suala hili na pia tuweze kupinga vikali vitendo kama hivi vya ulawiti na ubakaji ili kaunti ya Kwale tuwe na amani na tuweze kuendelea pamoja”, alisema Askofu Mwero.

Wakati huo huo amesema kama Kanisa wataendeleza hamasa za amani kwa jamii mashinani ili kuwaepusha vijana na visa vya uchochezi na migogoro ya kisiasa kutoka kwa baadhi ya wanasiasa wasiojali maslahi ya wananchi.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending