News
Kenyatta awarai wanachama wa Jubilee kuwa na fikra pana
Rais mstaafu Uhuru Kenyatta amewarai wafuasi na wanachama wa Chama cha Jubilee kuwa na fikra pana katika kuwachagua viongozi walio na maono ya maendeleo ili kufanikisha ajenda ya wananchi.
Kenyatta alisema kila mmoja na haki ya kupigania nafasi ya urais, bila kujali kabila, mrengo ama maeneo bali kwa kujali misingi ya ajenda ya maendeleo ya taifa, akisema kiongozi bora ni yule asiyepora na kutenga wengine.
Akizungumza katika mkutano wa chama hicho Ijumaa tarehe 26 mwezi wa Septemba 2025 baadfa ya kuufungua rasmi jijini Nairobi, Kenyatta alisema atahakikisha tiketi ya chama inatolewa kwa haki na uwazi kwa wagombea wa nyadhfa mbalimbali ili kuhakikisha chama hicho kinapata viongozi bora.
Kenyatta aliahidi kushirikiana ipasavyo na wanachama wa chama hicho kuhakikisha kinazidi kuwa imara huku Jubilee ikipendekeza Fred Matiang’I kupeperusha bendera ya jubilee kuwania wadhifa wa urais 2027.
“Kuanzia sasa nitakuwa nanyi tukizuru mashinani kwa lengo la kuimarisha chama chetu na nawasisi tudumishe umoja kama alivyosema Kioni’’, alisema Uhuru Kenyatta.

Rais mstaafu Uhuru Kenyatta, Katibu mkuu wa Jubilee Jeremiah Kioni, aliyekuwa Waziri wa usalama Fred Matiangi na viongozi wengine wakati wa mkutano wa chama cha Jubilee, Nairobi.
Kwa upande wake Katibu wa chama cha Jubilee nchini Jeremiah Kioni aliwahimiza wanachama wa chama cha Jubilee kuwa na umoja kwa ajili ya kipute cha uchaguzi mkuu ujao wa 2027.
Kioni alisema kuna baadhi ya changamoto ambazo ziliikumba chama hicho wakati na baada ya kuandaliwa kwa uchaguzi wa mwaka uliopita na ni lazima mikakati ifaayo iwekwe ili kushinda nyadhifa nyingi za uongozi 2027.
Kioni alisema kuna baadhi ya wanachama wa chama cha Jubilee ambao walichangia kwa chama hicho kuwa na migawanyiko na katiba ya chama itafanyiwa marekebisho ili kuhakikisha Jubilee iko thabiti.
“Ni lazima turekebishe katiba ya chama kama njia mojawapo ya maandalizi ya uchaguzi huo, maana kuna baadhi ya watu ambao hawakuwa wanaheshimu uongozi wa chama na walisababisha migawanyiko chamani’’ alisema Kioni.
Taarifa ya Janet Mumbi
News
Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA
Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane
Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.
Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.
Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.
“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.
News
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma
Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.
Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.
Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.
Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.
“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi
Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

