Connect with us

News

Wahuni watatiza maandamano ya vijana Nairobi

Published

on

Maandamano ya vijana  wa Gen Z jijini Nairobi wanaoshinikiza Naibu Inspekta jenerali wa polisi Eliud Lagat kujiuzulu yalikumbwa na changamoto baada kundi la vijana wahuni kuingilia kati na kuyatatiza.

Waandamanaji hao walilazimika kukimbilia usalama wao wakati magenge ya vijana waliokuwa kwenye bodaboda walipowakabili.

Wahuni hao walifika kwa kishindo wakiwa kwenye pikipiki kadhaa na kuwazuia vijana waliokuwa wakiandamana kwa amani kuelekea kituo kikuu cha polisi kwenye makutano ya University Way.

Waandamanaji waliwacha kambi pinzani kuchukua udhibiti na kutawala huku wakiondoka na kuwachapa viboko waliosalia barabarani.

Magari ya polisi na maafisa wa usalama walionekana wakishuhudia jinsi magenge hayo yalivyokuwa yakiwakimbiza na kuwafanyia fujo waandamanaji.

Hapo awali, polisi walikuwa wametumia vitoa machozi kutawanya umati uliokuwa umekusanyika katika kituo cha Nation ambapo ghadhabu ilianza.

Mvutano huo ulilemaza shughuli za biashara ndani ya jiji la Nairobi na maduka kufungwa huku Waandamanaji hao wakifanikiwa kutekeleza pikipiki ya wahuni hao.

Lagat alitangaza kujiuzuli kwa mda siku ya Jumatatu 16, Juni 2025 kufuatia shinikizo za vijana, wanaharakati wa kutetea haki za binadamu na viongozi wa kisiasa baada ya kuhusishwa na kifo cha mwanablogu Albert Ojwang. 

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kaunti ya Kilifi yatenga shilingi milioni 10 kusimamia wajane kwa SHA

Published

on

By

Serikali ya kaunti ya Kilifi imedai kwamba imetenga shilingi milioni 10 kusimamia huduma za afya kwa wajane

Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro aliwataka wajane na wanawake ambao bado hawajajisajili katika SHA, kutumia fursa hiyo ili iwe rahisi kwao kupata huduma za matibabu hospitalini.

Mung’aro aliwataka Wanawake wa kaunti ya Kilifi kuanza mchakato wa kuwasajali wajane katika SHA, akisema serikali ya kaunti iko na mipango ya kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma za matibabu bila changamoto.

Kiongozi hiyo pia alisema mikakati mwafaka imeidhinishwa kuhakikisha changamoto za urithi wa mashamba kwa akina wajane inashughulikiwa kupitia mawakili wa serikali ya kaunti.

“Naibu wangu ni mama, tuko na maafisa watano ni mama, kwa hivyo ni wajapange washirikiane na mawakili wa kaunti ili kupata haki ya urithi na tumetenga shilingi milioni 10 kusaidia wajane kujiandikisha na SHA ili wapate huduma za matibabu bila changamoto”,alisema Mung’aro.

Continue Reading

News

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki kwa umma

Published

on

Serikali imepiga marufuku uagizaji wa dawa za Antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda katika makaazi ya umma, ikisema mwenendo huo hautakubalika.

Waziri wa Afya nchini Adan Duele amesema serikali kupitia Wizara ya Afya nchini na Bodi ya dawa na sumu nchini zimeweka mikakati mwafaka ya kulinda afya ya wananchi.

Duale alisema wakenya hawafai kuilaumu bodi ya dawa na sumu nchini kutokana na sheria ngumu ilizotoa bali kuridhia hatua hiyo ili kuzuia madhara.

Akizungumza wakati wa warsha ya mikakati ya kuboresha afya ya umma, Waziri Duale alisema hatua hiyo inaanza kutekelezwa mara moja, huku akisisitiza kwamba serikali haitalegeza kambi katika kulinda afya ya umma.

“Kuanzia sasa hakuna tena kuagiza dawa za antibiotiki na kusafirishwa na wahudumu wa bodaboda kwani hatua hiyo ni hatari, wewe uko nyumbani kisha unaagiza dawa sini hiyo ni hatari, na hakuna kulaumu bodi ya dawa na sumu nchini kwa sababu tumeweka sheria hiyo”, alisema Duale.

Warsha ya watafiti wa kisayansi iliyiofanyika jijini Nairobi

Waziri huyo wa Afya nchini alishikilia kwamba hatua waliochukua mwafaka kwani italinda afya ya wananchi, akiwaonya wale wanaoendeleza bishara hiyo haramu. kusababisha madhara.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

Trending